Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Mawaziri walisema kwamba Uingereza sasa haitatoa msaada wa pauni milioni 21. Taarifa zinazohusiana * Siasa Rwanda ilipewa msaada wa kiasi cha pauni milioni 16 mnamo mwezi Septemba, hata baada ya tashwishi kuwepo kuhusu tetesi kwamba ilikuwa inawaunga mkono wanamgambo wa M23 wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Serikali ya Uingereza ilikuwa imesema kwamba ingetoa kitita kingine cha pauni milioni 18 kwa ajili ya mahitaji ya kibandamu ya dharura huko Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo Makubaliano Sasa fedha hizo, ambazo zilikuwa zitolewe mwezi ujao, hazitatolewa tena kwa sababu serikali ya Rais Paul Kagame imekiuka makubaliano. Nyaraka ya Umoja wa Mataifa iliyofichuliwa inasema kwamba waziri wa ulinzi wa Rwanda ndiye anayewaamrisha waasi walioko huko. Mapigano hayo yamepingwa na nchi za kimataifa, huku Marekani na nchi kadhaa za Ulaya zikizuia msaada uliokuwa umepangwa kwa ajili ya Rwanda. Waziri Justine Greening wa Uingereza alisema: “Nimeamua kutotoa fedha zilizokuwa zimekusidiwa kwa ajili ya kuisaidia bajeti ya Rwanda. Ni wajibu wetu kujaribu kutafuta suluhu za kudumu kwa mzozo wa eneo hili, na kufanya kazi pamoja na serikali za Rwanda na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo ili kuhakikisha suluhisho la amani linapatikana mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo."
Popular Posts
-
JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Cha...
-
Rais Dk.Kikwete akisimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wabena katika sherehe za kuzindua mkoa mpya ...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Mtaalamu kutoka Finland asaidia mikakati ya tehama
-
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali mtoto Andrew Simba(15) aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wakati Rais alipowate...
-
Marekani imo katika shughuli za kuwakumbuka waliokufa katika mashambulio ya Septemba 11, miaka 10 iliyopita, katika miji ya Washington na P...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), imezikutanisha kampuni za mafuta hapa nchini kwa lengo kuunda Bodi ya Wakurugenzi ya Kampu...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment