BALOZI wa Palestina hapa nchini, Dk Nasri Abujaish amesema ushindi iliyoupata nchi yake baada ya kupigiwa kura na hatimaye kuipandisha hadhi ni ushindi wa dunia nzima katika kupigania haki za binadamu, uhuru na amani. Dk Abujaish aliyasema hayo juzi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za ubalozi huo, zilizopo Upanga ,jijini Dar es Salaam. “Huu ni ushindi wa dunia nzima kwa ajili ya haki za binadamu, uhuru, utaifa na amani. Kwa hili ulimwengu useme sasa ‘yatosha kwa utawala na ukandamizaji’,” alisema Dk Abujaish. Hivi karibuni Baraza la Umoja wa Mataifa lilipitisha kwa kauli moja kwa wingi wa kura, kupandisha hadhi ya eneo la Palestina baada ya nchi 138 kuunga mkono hatua ya kuitambua Palestina kuwa nchi ambayo si mwanachama wa Umoja wa Mataifa lakini itaruhusiwa kushiriki katika shughuli za umoja huo. Hata hivyo mataifa tisa yakijumuisha Israel na Marekani yalipiga kura ya kupinga mpango huo, huku mataifa 41 yakisusia shughuli hiyo. Kura hiyo yenye umuhimu mkubwa, sasa inaiwezesha Palestina kuwa na ushirika katika Umoja wa Mataifa na mashirika mengine kama vile Mahakama ya ICC. Alisema baada ya hatua hiyo, Palestina itakuwa na uwezo wa kuzitumia mamlaka za Umoja wa Mataifa na Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita na inaweza kuishtaki Israel kutokana na vitendo vyake vilivyo kinyume cha haki za binadamu. Alisema chini ya hatua hiyo, wafungwa wa kisiasa watakuwa wakichukuliwa kama wafungwa wa vita chini ya Azimio la nne la Geneva. “Kutokana na ushindi huo, uvamizi wa Israel unakuwa umekataliwa na Taifa la Palestina limeshinda. Tunatumai kuwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litakubali ombi la Palestina lililowasilishwa mwaka 2011 la kuipa uanachama wa moja kwa moja na kufikia mwafaka wa mipaka ya nchi mbili ulioanza tangu mwaka 1967,” alisema. Alisema ushindi huo pia utawawezesha kutafuta suluhisho kati yake na Israel kuhusu matamko yaliyokiuka sheria, Mji wa Jerusalem, mipaka, wakimbizi maji na rasilimali nyinginezo. “Nazishukuru nchi 138 zilizoipigia kura Palestina, zinatoka Afrika, Asia, Marekani Kusini na sehemu ya Ulaya. Kwa kipekee kabisa tunaishukuru Tanzania kwa kusimama upande wetu. Kwa mara nyingine imeonyesha mshikamano wa kihistoria uliokuwepo,” alisema. Kuhusu mataifa yaliyopiunga mpango huo, Dk Abujaish alisema yanakwenda kinyume na kanuni za haki za binadamu zinazodai kuzipigania. Kwa muda mrefu sasa, Palestina imekuwa ikishinikiza kutambuliwa kuwa ni taifa huru, lakini imekuwa ikipata vipingamizi kutoka Marekani na washirika wake ikiwamo Israeli. Hata hivyo kiongozi wa palestina Mahamood Abbas, ameapa kuendelea na jiotihada za kuushinikiza Umoja wa Mataifa na mataifa mengine duniani, ili yakubali kuitambua Palestina. Nchi hiyo imekuwa ikipinga vikali utawala wa mabavu wa Israel ambayo imekuwa ikikalia baadhi ya maeneo yake, jambo linalosababisha kukua kwa mgogoro wa mara kwa mara. Hata hivyo mataifa mbalimbali duniani yamekuwa yakihimiza amani.
Popular Posts
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Arsenal imemsajili winga wa Southampton Alex Oxlade-Chamberlain kwa ada inayoaminika ni paundi milioni 15. Mchezaji huyo mwenye umri wa m...
-
ZANZIBAR imo hatarini kukabiliwa na janga kubwa la uharibifu wa mazingira ya bahari iwapo kasi ya uingizaji mifuko ya plastiki itaendelea, ...
-
Tanzania imetangaza kuwa inapiga marufuku biashara ya kukamata na kuwasafirisha wanyamapori kwenda nje ya nchi. Hatua hiyo imetangazwa na...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
Wazalishaji na wasambazaji wa nishati ya gesi kutoka Kisiwa cha Songosongo, SONGAS wameishauri serikali kuwashirikisha wadau wengine ikiwem...
-
Balozi Seif Ai Iddi (kulia) ambaye ni makamu wa pili wa rais wa zanzibar na mbunge wa jimbo la kitope kaskazini unguja akizungumza na spika...
-
MBIO za kuwatafuta vinara watatu wa mastaa wa shindano la Tusker Project Fame, waliowahi kushiriki miaka minne iliyopita zitafikia ukingoni...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment