BALOZI wa Palestina hapa nchini, Dk Nasri Abujaish amesema ushindi iliyoupata nchi yake baada ya kupigiwa kura na hatimaye kuipandisha hadhi ni ushindi wa dunia nzima katika kupigania haki za binadamu, uhuru na amani. Dk Abujaish aliyasema hayo juzi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za ubalozi huo, zilizopo Upanga ,jijini Dar es Salaam. “Huu ni ushindi wa dunia nzima kwa ajili ya haki za binadamu, uhuru, utaifa na amani. Kwa hili ulimwengu useme sasa ‘yatosha kwa utawala na ukandamizaji’,” alisema Dk Abujaish. Hivi karibuni Baraza la Umoja wa Mataifa lilipitisha kwa kauli moja kwa wingi wa kura, kupandisha hadhi ya eneo la Palestina baada ya nchi 138 kuunga mkono hatua ya kuitambua Palestina kuwa nchi ambayo si mwanachama wa Umoja wa Mataifa lakini itaruhusiwa kushiriki katika shughuli za umoja huo. Hata hivyo mataifa tisa yakijumuisha Israel na Marekani yalipiga kura ya kupinga mpango huo, huku mataifa 41 yakisusia shughuli hiyo. Kura hiyo yenye umuhimu mkubwa, sasa inaiwezesha Palestina kuwa na ushirika katika Umoja wa Mataifa na mashirika mengine kama vile Mahakama ya ICC. Alisema baada ya hatua hiyo, Palestina itakuwa na uwezo wa kuzitumia mamlaka za Umoja wa Mataifa na Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita na inaweza kuishtaki Israel kutokana na vitendo vyake vilivyo kinyume cha haki za binadamu. Alisema chini ya hatua hiyo, wafungwa wa kisiasa watakuwa wakichukuliwa kama wafungwa wa vita chini ya Azimio la nne la Geneva. “Kutokana na ushindi huo, uvamizi wa Israel unakuwa umekataliwa na Taifa la Palestina limeshinda. Tunatumai kuwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa litakubali ombi la Palestina lililowasilishwa mwaka 2011 la kuipa uanachama wa moja kwa moja na kufikia mwafaka wa mipaka ya nchi mbili ulioanza tangu mwaka 1967,” alisema. Alisema ushindi huo pia utawawezesha kutafuta suluhisho kati yake na Israel kuhusu matamko yaliyokiuka sheria, Mji wa Jerusalem, mipaka, wakimbizi maji na rasilimali nyinginezo. “Nazishukuru nchi 138 zilizoipigia kura Palestina, zinatoka Afrika, Asia, Marekani Kusini na sehemu ya Ulaya. Kwa kipekee kabisa tunaishukuru Tanzania kwa kusimama upande wetu. Kwa mara nyingine imeonyesha mshikamano wa kihistoria uliokuwepo,” alisema. Kuhusu mataifa yaliyopiunga mpango huo, Dk Abujaish alisema yanakwenda kinyume na kanuni za haki za binadamu zinazodai kuzipigania. Kwa muda mrefu sasa, Palestina imekuwa ikishinikiza kutambuliwa kuwa ni taifa huru, lakini imekuwa ikipata vipingamizi kutoka Marekani na washirika wake ikiwamo Israeli. Hata hivyo kiongozi wa palestina Mahamood Abbas, ameapa kuendelea na jiotihada za kuushinikiza Umoja wa Mataifa na mataifa mengine duniani, ili yakubali kuitambua Palestina. Nchi hiyo imekuwa ikipinga vikali utawala wa mabavu wa Israel ambayo imekuwa ikikalia baadhi ya maeneo yake, jambo linalosababisha kukua kwa mgogoro wa mara kwa mara. Hata hivyo mataifa mbalimbali duniani yamekuwa yakihimiza amani.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment