WAKATI mpango wa mwaka mmoja wa umeme wa dharura ukiwa umemalizika, utekelezaji wake umeshindwa kufikiwa na matokeo yake tatizo la mgawo umeme usiotabirika linaendelea nchini. Serikali na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wameshindwa kutoa majibu sahihi kuhusiana na kukwama kwa mradi huo. Alipoulizwa kuhusu maendeleo ya mpango huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alisema, “Leo ni Jumamosi, nipo kanisani. Naomba uniache kwanza, tena nisingependa kuzungumzia suala hilo kabisa.” Gazeti hili lilimtafuta Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kwa njia ya simu lakini hakupokea na badala yake alituma ujumbe mfupi wa maneno uliosomeka, “I am in meeting (nipo kwenye mkutano).” Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Tanesco, Felschami Mramba alisema kuwa haiwezekani kukawa na mpango wa dharura wa mwaka mmoja akieleza kuwa madhara humalizika tatizo husika linapokuwa limekwisha. “Huu mpango wa dharura utakwisha siku ambayo bomba la gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme litakapofika Dar es Salaam likitokea Mtwara,” alisema. Waziri Muhongo Akiwasilisha bajeti ya wizara yake katika Bunge la Bajeti mwaka huu, Profesa Sospeter Muhongo alisema kuwa wizara yake imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme nchini. Alisema hadi Juni 2012 uwezo wa mitambo ya kufua umeme ulikuwa megawati 1,375.74, gesi asili asilimia 40, maji ( 41) na mafuta (19). Alieleza kuwa uwezo huo ni ongezeko la megawati 367 sawa na asilimia 36 ikilinganishwa na uwezo wa megawati 1,013.74 uliokuwapo Juni, 2011. Mahitaji ya juu ya umeme kwa mwaka 2011/12 yalifikia wastani wa megawati 820.35, ikilinganishwa na megawati 730 kwa mwaka 2010/11. Uhaba huo wa umeme ndiyo ulizaa Mpango wa Dharura wa Kuondoa Mgawo wa Umeme nchini ulioridhiwa na Bunge. Katika Mpango huo, jumla ya megawati 572 zilipangwa kuzalishwa na kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa. Mitambo iliyotumika kuzalishia umeme huo ni Symbion megawati 137, Aggreko (100), IPTL (80) na ule wa Gesi Asili wa Ubungo (105).
Popular Posts
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itafanya kila juhudi kuhakikisha...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amewapiga marufuku wafanyakazi wote walio chini ya wizara yake kusafiri kwa ndege katika daraja...
-
Dar es Salaam. Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka amesema mwezi ujao wanatarajia kutangaza kima cha chini cha mshahara kwa wafany...
-
JAJI MKUU AELEZA SABABU ZA KUJITOA KESI YA LEMA JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji wali...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
WAKATI mpango wa mwaka mmoja wa umeme wa dharura ukiwa umemalizika, utekelezaji wake umeshindwa kufikiwa na matokeo yake tatizo la mgaw...
-
AFRICA has made remarkable progress in fighting malaria under alliance championed by President Jakaya Kikwete, but the success was describe...
-
NEEMA imeendelea kumdondokea mwanamuziki Chaz Baba ambaye baada ya kuhamia Bendi ya Mashujaa Musica na kuvuta mkwanja mrefu, sasa amechag...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment