WAKATI mpango wa mwaka mmoja wa umeme wa dharura ukiwa umemalizika, utekelezaji wake umeshindwa kufikiwa na matokeo yake tatizo la mgawo umeme usiotabirika linaendelea nchini. Serikali na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wameshindwa kutoa majibu sahihi kuhusiana na kukwama kwa mradi huo. Alipoulizwa kuhusu maendeleo ya mpango huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alisema, “Leo ni Jumamosi, nipo kanisani. Naomba uniache kwanza, tena nisingependa kuzungumzia suala hilo kabisa.” Gazeti hili lilimtafuta Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kwa njia ya simu lakini hakupokea na badala yake alituma ujumbe mfupi wa maneno uliosomeka, “I am in meeting (nipo kwenye mkutano).” Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Tanesco, Felschami Mramba alisema kuwa haiwezekani kukawa na mpango wa dharura wa mwaka mmoja akieleza kuwa madhara humalizika tatizo husika linapokuwa limekwisha. “Huu mpango wa dharura utakwisha siku ambayo bomba la gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme litakapofika Dar es Salaam likitokea Mtwara,” alisema. Waziri Muhongo Akiwasilisha bajeti ya wizara yake katika Bunge la Bajeti mwaka huu, Profesa Sospeter Muhongo alisema kuwa wizara yake imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme nchini. Alisema hadi Juni 2012 uwezo wa mitambo ya kufua umeme ulikuwa megawati 1,375.74, gesi asili asilimia 40, maji ( 41) na mafuta (19). Alieleza kuwa uwezo huo ni ongezeko la megawati 367 sawa na asilimia 36 ikilinganishwa na uwezo wa megawati 1,013.74 uliokuwapo Juni, 2011. Mahitaji ya juu ya umeme kwa mwaka 2011/12 yalifikia wastani wa megawati 820.35, ikilinganishwa na megawati 730 kwa mwaka 2010/11. Uhaba huo wa umeme ndiyo ulizaa Mpango wa Dharura wa Kuondoa Mgawo wa Umeme nchini ulioridhiwa na Bunge. Katika Mpango huo, jumla ya megawati 572 zilipangwa kuzalishwa na kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa. Mitambo iliyotumika kuzalishia umeme huo ni Symbion megawati 137, Aggreko (100), IPTL (80) na ule wa Gesi Asili wa Ubungo (105).
Popular Posts
-
Company ya Globalwisesoftnet Tanzania, ime sign Contract na Company ya Google pamoja na Microsoft, kwa lengo la kuendeleza na kubuni mbinu ...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Arsenal imemsajili winga wa Southampton Alex Oxlade-Chamberlain kwa ada inayoaminika ni paundi milioni 15. Mchezaji huyo mwenye umri wa m...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
Balozi Seif Ai Iddi (kulia) ambaye ni makamu wa pili wa rais wa zanzibar na mbunge wa jimbo la kitope kaskazini unguja akizungumza na spika...
-
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akionyshwa DJ Tasi (kushoto) anavyofanyakazi alipotembelea kituo cha Magic FM akaiwa katika z...
-
Kwa miaka 28 ukuta huo ulitenganisha upande wa mashariki uliokuwa chini ya utawala wa kikoministi na ule uliokuwa sehemu ya Ujerumani Mag...
-
Wazungu wawili raia wa Ujerumani, VEIXLAR MARLM (24), WEIXLER ROLAND (21) wamenusurika kuuawa baada ya kutekwa na watu waliojifanya waendes...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment