WAKATI mpango wa mwaka mmoja wa umeme wa dharura ukiwa umemalizika, utekelezaji wake umeshindwa kufikiwa na matokeo yake tatizo la mgawo umeme usiotabirika linaendelea nchini. Serikali na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wameshindwa kutoa majibu sahihi kuhusiana na kukwama kwa mradi huo. Alipoulizwa kuhusu maendeleo ya mpango huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alisema, “Leo ni Jumamosi, nipo kanisani. Naomba uniache kwanza, tena nisingependa kuzungumzia suala hilo kabisa.” Gazeti hili lilimtafuta Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kwa njia ya simu lakini hakupokea na badala yake alituma ujumbe mfupi wa maneno uliosomeka, “I am in meeting (nipo kwenye mkutano).” Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Tanesco, Felschami Mramba alisema kuwa haiwezekani kukawa na mpango wa dharura wa mwaka mmoja akieleza kuwa madhara humalizika tatizo husika linapokuwa limekwisha. “Huu mpango wa dharura utakwisha siku ambayo bomba la gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme litakapofika Dar es Salaam likitokea Mtwara,” alisema. Waziri Muhongo Akiwasilisha bajeti ya wizara yake katika Bunge la Bajeti mwaka huu, Profesa Sospeter Muhongo alisema kuwa wizara yake imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme nchini. Alisema hadi Juni 2012 uwezo wa mitambo ya kufua umeme ulikuwa megawati 1,375.74, gesi asili asilimia 40, maji ( 41) na mafuta (19). Alieleza kuwa uwezo huo ni ongezeko la megawati 367 sawa na asilimia 36 ikilinganishwa na uwezo wa megawati 1,013.74 uliokuwapo Juni, 2011. Mahitaji ya juu ya umeme kwa mwaka 2011/12 yalifikia wastani wa megawati 820.35, ikilinganishwa na megawati 730 kwa mwaka 2010/11. Uhaba huo wa umeme ndiyo ulizaa Mpango wa Dharura wa Kuondoa Mgawo wa Umeme nchini ulioridhiwa na Bunge. Katika Mpango huo, jumla ya megawati 572 zilipangwa kuzalishwa na kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa. Mitambo iliyotumika kuzalishia umeme huo ni Symbion megawati 137, Aggreko (100), IPTL (80) na ule wa Gesi Asili wa Ubungo (105).
Popular Posts
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
KAMPUNI ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti imetoa msaada wa kilo 200 ...
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasafisha aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi ...
-
UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Maha...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment