WAKATI mpango wa mwaka mmoja wa umeme wa dharura ukiwa umemalizika, utekelezaji wake umeshindwa kufikiwa na matokeo yake tatizo la mgawo umeme usiotabirika linaendelea nchini. Serikali na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) wameshindwa kutoa majibu sahihi kuhusiana na kukwama kwa mradi huo. Alipoulizwa kuhusu maendeleo ya mpango huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alisema, “Leo ni Jumamosi, nipo kanisani. Naomba uniache kwanza, tena nisingependa kuzungumzia suala hilo kabisa.” Gazeti hili lilimtafuta Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kwa njia ya simu lakini hakupokea na badala yake alituma ujumbe mfupi wa maneno uliosomeka, “I am in meeting (nipo kwenye mkutano).” Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Tanesco, Felschami Mramba alisema kuwa haiwezekani kukawa na mpango wa dharura wa mwaka mmoja akieleza kuwa madhara humalizika tatizo husika linapokuwa limekwisha. “Huu mpango wa dharura utakwisha siku ambayo bomba la gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme litakapofika Dar es Salaam likitokea Mtwara,” alisema. Waziri Muhongo Akiwasilisha bajeti ya wizara yake katika Bunge la Bajeti mwaka huu, Profesa Sospeter Muhongo alisema kuwa wizara yake imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme nchini. Alisema hadi Juni 2012 uwezo wa mitambo ya kufua umeme ulikuwa megawati 1,375.74, gesi asili asilimia 40, maji ( 41) na mafuta (19). Alieleza kuwa uwezo huo ni ongezeko la megawati 367 sawa na asilimia 36 ikilinganishwa na uwezo wa megawati 1,013.74 uliokuwapo Juni, 2011. Mahitaji ya juu ya umeme kwa mwaka 2011/12 yalifikia wastani wa megawati 820.35, ikilinganishwa na megawati 730 kwa mwaka 2010/11. Uhaba huo wa umeme ndiyo ulizaa Mpango wa Dharura wa Kuondoa Mgawo wa Umeme nchini ulioridhiwa na Bunge. Katika Mpango huo, jumla ya megawati 572 zilipangwa kuzalishwa na kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa. Mitambo iliyotumika kuzalishia umeme huo ni Symbion megawati 137, Aggreko (100), IPTL (80) na ule wa Gesi Asili wa Ubungo (105).
Popular Posts
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
BAADHI ya wananchi wa Ubungo katika Manispaa ya Kinondoni, jana wavamia Ofisi za Kampuni inayosambaza maji katika Jiji la Dar es Salaam na...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
Chimbuko la uvujaji wa mitihani nchini Tanzania lina historia ndefu inayoenda sambamba na kuundwa kwa BARAZA LA MITIHANI LA TAI...
-
RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni amewapandisha vyeo maofisa wa juu wa jeshi pamoja na kuwahamisha baadhi ya maofisa akiwemo mlinzi wake mk...
-
I: UTANGULIZI a) Masuala ya Jumla Mheshimiwa Spika, 1. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi M...
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK.Jakaya kikwete akilihutubia bunge mjini Dodoma.kulia ni spika wa Bunge Anne Makinda. Wab...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment