MIONZI ya simu za mkononi inaweza kuathiri maendeleo ya ubongo wa watoto walioko tumboni mwa mama zao, utafiti umeeleza.Utafiti huo umetaja madhara mengine ya mionzi ya simu za mkononi kuwa ni uharibifu wa manii, mimba, kupungua kwa nguvu za kiume, kupoteza kumbukumbu na kuzaa watoto watukutu. Pia umeeleza kuwa matumizi kupita kiasi ya simu hizo, husababisha mtindio wa ubongo na upungufu wa udadisi kwa watoto tangu udogo wao. Hata hivyo, utafiti huo uliofanywa na Shule ya Tiba na Dawa ya Chuo Kikuu cha Yale, Marekani na kuripotiwa na Gazeti la The Telegraph la Uingereza, umepingwa na watafiti wengine, wakisema haujakidhi baadhi ya vigezo ili kuuthibitisha. Kiongozi wa jopo la utafiti huo, Profesa Hugh Taylor alisema utafiti huo ulioanzia kwa panya, baadaye ulithibitika kwa binadamu. Profesa Taylor ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Uzazi, Magonjwa ya Wanawake na Sayansi ya Uzazi, alisema: “Tulikuwa na panya wenye mimba katika maboksi na tuliwawekea simu juu ya vichwa vyao. Panya tuliokuwa tumewaweka katika bwawa lile, nusu yao walikuwa wazima na nusu yao walikufa. Panya waliokuwa hai tuliwaacha wajifungue na baada ya kujifungua, tukaanza kutafiti watoto wao.” “Panya ambao hawakuwa karibu na simu za mikononi walionekana kuwa werevu. Kumbukumbu zao hazikupungua ikilinganishwa na panya walioathiriwa na mionzi ya simu za mikononi ambao katika vipimo vya awali wakiwa tumboni, walionekana kuhangaika.” “Panya hao wenye mimba waliowekwa kwa siku 17 katika boksi hilo na simu kupigwa mfululizo juu ya vichwa vyao, walizaa watoto watukutu na waliokosa kumbukumbu.” Aliongeza: “Matokeo hayo yanaweza kutokea kwa binadamu pia. Mjamzito anayetumia simu ya mkononi muda mwingi, anaweza pia kuzaa taahira.”
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment