Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itafanya kila juhudi kuhakikisha kwamba maharibiko ya kuanguka sehemu ya jengo la Makumbusho ya Taifa Beit El Ajab yanarekebishwa na matengenezo ya jumla ya jengo hilo na majengo yote ya kihistoria yanasimamiwa ipasavyo. Akizungumza na waandishi wa habari katika makumbusho ya Mnazimmoja, Waziri Mbarouk amesema kutokana na heshima na hadhi ya jengo la Beit El Ajab kwa historia ya Zanzibar, kuanguka kwa jengo hilo kumeathiri shughuli za utalii kwani ni miongoni mwa vivutio vikuu vya Utalii ZANZIBAR. “Asilimia 70 ya wageni wanaotembelea sehemu za kihistoria huwa wanafika makumbusho ya Beit El Ajab’’, alisema Waziri Said Ali Mbarouk. Amesema uamuzi wa kuyahifadhi maeneo ya Historia ikiwemo jengo la Beit El Ajab utaendelea kupewa umuhimu mkubwa kwani ni sehemu ya urithi wa Utamaduni wa Zanzibar na yanahitaji kudumu kwa miaka mingi zaidi. “Jengo hili lililojengwa mwaka 1883 na Mfalme Barghash bin Said ni moja kati ya majengo yenye hadhi kubwa kihistoria, kijamii, kiuchumi na kisiasa kwa Zanzibar” alisisitiza Waziri Mbarouk. Amesema umaarufu wa jengo la Beit El Ajab unatokana na kuwa ni la kwanza Zanzibar kuwekewa huduma za kijamii kama vile umeme, simu, lifti na maji ya mfereji kabla ya huduma hizo hazijaanzishwa kwenye nchi nyingi za Afrika Mashariki. Ameongeza kuwa kutokana na maharibiko yaliyotokea Mamlaka ya Uhifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe inachukua hatua ya kuiarifu UNESCO kuhusu tukio hilo na kuomba msaada wa kitaalamu na fedha kulinusuru. Aidha amesema Idara ya Makumbusho na Mambo ya kale inafanya mawasiliano na watalaalamu wa majengo ya kale ili kupata tathmini ya hali ya jengo hilo na Kasri ya Kifalme na aina ya matengenezo ya kudumu na gharama zinazohitajika. Jengo la Makumbusho kuu ya Jumba la Ajab lilianguka usiku wa Jumamosi iliyopita wakati likiendelea kufanyiwa matengenezo na MACEMP na limewahi kutumika kwa sherehe na shughuli za utawala wakati wa ufalme, Makumbusho ya Chama cha ASP, Chuo cha Itikadi ya Chama na kuanzia mwaka 2002 likapewa hadhi ya kuwa makumbusho inayohusu Utamaduni wa Mswahili na Historia ya Zanzibar.
Popular Posts
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
BAADHI ya wananchi wa Ubungo katika Manispaa ya Kinondoni, jana wavamia Ofisi za Kampuni inayosambaza maji katika Jiji la Dar es Salaam na...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
Chimbuko la uvujaji wa mitihani nchini Tanzania lina historia ndefu inayoenda sambamba na kuundwa kwa BARAZA LA MITIHANI LA TAI...
-
RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni amewapandisha vyeo maofisa wa juu wa jeshi pamoja na kuwahamisha baadhi ya maofisa akiwemo mlinzi wake mk...
-
I: UTANGULIZI a) Masuala ya Jumla Mheshimiwa Spika, 1. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi M...
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK.Jakaya kikwete akilihutubia bunge mjini Dodoma.kulia ni spika wa Bunge Anne Makinda. Wab...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)



0 comments:
Post a Comment