RAIS Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo maofisa wakuu kutoka cheo cha Meja Jenerali kuwa Luteni Jenerali kuanzia Novemba 21,mwaka huu. Kwa mujibu ya taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), inaeleza kuwa maofisa wakuu waliopandishwa cheo ni Meja Jenerali, Sylvester Chacha Ryoba ambaye ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Maafa ofisi ya Waziri Mkuu kuwa Luteni Jenerali. Mwingine ni Meja Jenerali, Charles Lawrance Makakala ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi. Rais Kikwete na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange amewapongeza wakuu hao. Wakati huohuo, Rais Jakaya Kikwete kesho anatarajia kufanya ziara ya siku moja mjini Rufiji, licha ya mambo mengine atahutubia mkutano wa hadhara mjini Ikwiriri. Akizungumza jana kwenye Baraza la Madiwani, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji, Leonard Rwegasira alisema Rais Kikwete atapokelewa mpakani mwa wilaya ya Kilwa na Rufiji, eneo la Malendego. Rwegasira alisema wananchi wa Rufiji wametakiwa kujitokeza kwa wingi kumpokea kiongozi huyo atakapoingia wilayani hapa ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mwaka 2010. Hata hivyo, Rwegasira aliwataka madiwani kuwajulisha wananchi kushiriki kumpokea.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment