RAIS Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo maofisa wakuu kutoka cheo cha Meja Jenerali kuwa Luteni Jenerali kuanzia Novemba 21,mwaka huu. Kwa mujibu ya taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), inaeleza kuwa maofisa wakuu waliopandishwa cheo ni Meja Jenerali, Sylvester Chacha Ryoba ambaye ni Mkurugenzi wa Kitengo cha Maafa ofisi ya Waziri Mkuu kuwa Luteni Jenerali. Mwingine ni Meja Jenerali, Charles Lawrance Makakala ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi. Rais Kikwete na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange amewapongeza wakuu hao. Wakati huohuo, Rais Jakaya Kikwete kesho anatarajia kufanya ziara ya siku moja mjini Rufiji, licha ya mambo mengine atahutubia mkutano wa hadhara mjini Ikwiriri. Akizungumza jana kwenye Baraza la Madiwani, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji, Leonard Rwegasira alisema Rais Kikwete atapokelewa mpakani mwa wilaya ya Kilwa na Rufiji, eneo la Malendego. Rwegasira alisema wananchi wa Rufiji wametakiwa kujitokeza kwa wingi kumpokea kiongozi huyo atakapoingia wilayani hapa ikiwa ni ziara yake ya kwanza tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mwaka 2010. Hata hivyo, Rwegasira aliwataka madiwani kuwajulisha wananchi kushiriki kumpokea.
Popular Posts
-
JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Cha...
-
Rais Dk.Kikwete akisimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wabena katika sherehe za kuzindua mkoa mpya ...
-
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya waombolezaji baada a kuwasili nyumbani kwa aliyekuwa Wazri wa Fedha, Dr. ...
-
MFUMUKO wa bei unaweza kuwakimbiza wawekezaji wanaotaka kuja nchini kuwekeza rasilimali zao kama utaendelea kukua kama ilivyo sasa.Kwa s...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), imezikutanisha kampuni za mafuta hapa nchini kwa lengo kuunda Bodi ya Wakurugenzi ya Kampu...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo jipya la K...
-
DHANA ya kwamba Tanzania tumekuwa hatufaidi maliasili zetu kama vile utalii, madini , pamoja na mlima Kilimanjaro, na badala yake fursa...
-
Ujerumani imerejesha mafuvu ya Wanambia ishirini waliofariki dunia baada ya fujo dhidi ya utawala wa ukoloni wa Kijerumani zaidi ya miaka 1...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment