KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, ameonya kuhusu mpango wa Israeli kuhusiana na ujenzi wa makao mapya ya walowezi kwa kuhofia athari za upotevu wa amani. Ki-moon ameonyesha hali ya wasiwasi juu ya ujenzi ya huo na kusisitiza kuwa ujenzi huo usitishwe katika eneo hilo kwa kuwa endapo ujenzi huo utaendelea unaweza kuvuruga hali ya amani. “Mpango wowote wa kujenga makazi katika sehemu inayojulikana kama E1 ni lazima usitishwe kwa kuwa hatua hiyo itakuwa ni pigo kubwa katika fursa iliyopo ya mazungumzo ya amani,” alisema. Naye Mkuu wa sera katika Muungano wa Ulaya, Catherene Ashton, alielezea wasiwasi kuhusu mpango wa ujenzi wa makazi mengine ya walowezi na kuwataka kuachana na mpango wa ujenzi huo . Kauli hiyo imetolewa mara baada ya Israeli kusema mpango wao wa kuongeza nyumba elfu tatu kwa makazi yaliopo na inatarajia kuongeza makazi mapya kwa kuunganisha yale yaliyopo katika Ukingo wa Magharibi na Jerusalemu Mashariki. Israeli Ilitangaza mpango huo kufuatia kura ambayo iliyopigwa na Umoja wa Mataifa (UN) iliyoipandisha Palestina hadhi kuwa dola mwangalizi katika umoja huo. Kutokana na hali hiyo, Kiongozi wa Palestina, Mahmoud Abbas alipokewa kwa shangwe mjini Ramallah katika ukingo wa Magharibi aliporudi nyumbani kutoka kwenye mkutano huo ambao uliipa sifa taifa hilo kwa kupandishwa hadhi. Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ameahidi kuendelea na mpango wake wa ujenzi licha ya kuwepo kwa sintofahamu juu ya ujenzi huo.
Popular Posts
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
BAADHI ya wananchi wa Ubungo katika Manispaa ya Kinondoni, jana wavamia Ofisi za Kampuni inayosambaza maji katika Jiji la Dar es Salaam na...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
Chimbuko la uvujaji wa mitihani nchini Tanzania lina historia ndefu inayoenda sambamba na kuundwa kwa BARAZA LA MITIHANI LA TAI...
-
RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni amewapandisha vyeo maofisa wa juu wa jeshi pamoja na kuwahamisha baadhi ya maofisa akiwemo mlinzi wake mk...
-
I: UTANGULIZI a) Masuala ya Jumla Mheshimiwa Spika, 1. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi M...
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK.Jakaya kikwete akilihutubia bunge mjini Dodoma.kulia ni spika wa Bunge Anne Makinda. Wab...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment