KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, ameonya kuhusu mpango wa Israeli kuhusiana na ujenzi wa makao mapya ya walowezi kwa kuhofia athari za upotevu wa amani. Ki-moon ameonyesha hali ya wasiwasi juu ya ujenzi ya huo na kusisitiza kuwa ujenzi huo usitishwe katika eneo hilo kwa kuwa endapo ujenzi huo utaendelea unaweza kuvuruga hali ya amani. “Mpango wowote wa kujenga makazi katika sehemu inayojulikana kama E1 ni lazima usitishwe kwa kuwa hatua hiyo itakuwa ni pigo kubwa katika fursa iliyopo ya mazungumzo ya amani,” alisema. Naye Mkuu wa sera katika Muungano wa Ulaya, Catherene Ashton, alielezea wasiwasi kuhusu mpango wa ujenzi wa makazi mengine ya walowezi na kuwataka kuachana na mpango wa ujenzi huo . Kauli hiyo imetolewa mara baada ya Israeli kusema mpango wao wa kuongeza nyumba elfu tatu kwa makazi yaliopo na inatarajia kuongeza makazi mapya kwa kuunganisha yale yaliyopo katika Ukingo wa Magharibi na Jerusalemu Mashariki. Israeli Ilitangaza mpango huo kufuatia kura ambayo iliyopigwa na Umoja wa Mataifa (UN) iliyoipandisha Palestina hadhi kuwa dola mwangalizi katika umoja huo. Kutokana na hali hiyo, Kiongozi wa Palestina, Mahmoud Abbas alipokewa kwa shangwe mjini Ramallah katika ukingo wa Magharibi aliporudi nyumbani kutoka kwenye mkutano huo ambao uliipa sifa taifa hilo kwa kupandishwa hadhi. Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ameahidi kuendelea na mpango wake wa ujenzi licha ya kuwepo kwa sintofahamu juu ya ujenzi huo.
Popular Posts
-
Chimbuko la uvujaji wa mitihani nchini Tanzania lina historia ndefu inayoenda sambamba na kuundwa kwa BARAZA LA MITIHANI LA TAI...
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amewapiga marufuku wafanyakazi wote walio chini ya wizara yake kusafiri kwa ndege katika daraja...
-
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Sabas akiwaonyesha waandishi wa habari (Ha...
-
BALOZI wa Palestina hapa nchini, Dk Nasri Abujaish amesema ushindi iliyoupata nchi yake baada ya kupigiwa kura na hatimaye kuipandisha h...
-
JUMUIYA ya Ulaya (EU), imeongeza masharti kwa Serikali ya Tanzania ili iweze kupatiwa msaada wa Bajeti kwa mwaka ujao wa fedha 2013/14. ...
-
ALIYEKUWA Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi (DPA) wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Amatus Liyumba ambaye anatumikia kifungo cha miaka miwili je...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment