KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon, ameonya kuhusu mpango wa Israeli kuhusiana na ujenzi wa makao mapya ya walowezi kwa kuhofia athari za upotevu wa amani. Ki-moon ameonyesha hali ya wasiwasi juu ya ujenzi ya huo na kusisitiza kuwa ujenzi huo usitishwe katika eneo hilo kwa kuwa endapo ujenzi huo utaendelea unaweza kuvuruga hali ya amani. “Mpango wowote wa kujenga makazi katika sehemu inayojulikana kama E1 ni lazima usitishwe kwa kuwa hatua hiyo itakuwa ni pigo kubwa katika fursa iliyopo ya mazungumzo ya amani,” alisema. Naye Mkuu wa sera katika Muungano wa Ulaya, Catherene Ashton, alielezea wasiwasi kuhusu mpango wa ujenzi wa makazi mengine ya walowezi na kuwataka kuachana na mpango wa ujenzi huo . Kauli hiyo imetolewa mara baada ya Israeli kusema mpango wao wa kuongeza nyumba elfu tatu kwa makazi yaliopo na inatarajia kuongeza makazi mapya kwa kuunganisha yale yaliyopo katika Ukingo wa Magharibi na Jerusalemu Mashariki. Israeli Ilitangaza mpango huo kufuatia kura ambayo iliyopigwa na Umoja wa Mataifa (UN) iliyoipandisha Palestina hadhi kuwa dola mwangalizi katika umoja huo. Kutokana na hali hiyo, Kiongozi wa Palestina, Mahmoud Abbas alipokewa kwa shangwe mjini Ramallah katika ukingo wa Magharibi aliporudi nyumbani kutoka kwenye mkutano huo ambao uliipa sifa taifa hilo kwa kupandishwa hadhi. Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ameahidi kuendelea na mpango wake wa ujenzi licha ya kuwepo kwa sintofahamu juu ya ujenzi huo.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment