LOS ANGELES, Marekani MWANAMUZIKI Mary Jane Blige ni kati ya wanamuziki mahiri wa Marekani.Blige, aliyezaliwa Januari 11, 1971, pia anasifika kutokana na kuwa prodyuza na kucheza filamu. Ameshinda tuzo tisa za Grammy na American Music Award kutokana na muziki wa R&B, Rap, Gospel na Pop. Blige alianza muziki mwaka 1992 baada ya kutoa albamu ya kwanza aliyoipa jina la 'What's the 411'. Mwanamuziki huyo ameuza zaidi ya nakala milioni 50 za albamu za muziki sehemu mbalimbali duniani. Anahesabiwa kuwa miongoni mwa wanamuziki wa R&B wenye mafanikio zaidi katika kipindi cha miaka 25. Blige pia amejizolea sifa kubwa kutokana na kazi zake za filamu na manukato. Aling'ara katika filamu ya Tyler Perry iliyotolewa mwaka 2009. Mwanamuziki huyo anakadiriwa kuwa na utajiri wa kiasi cha Dola 45 milioni (Sh 70 bilioni). Mwaka 2004, alianzisha lebo ya Matriarch Records na amekuwa akisambaza kazi za wanamuziki mbalimbali. Pia anatengeneza manukato yanayoitwa My Life na My Life Blossom HSN. Blige pia ana kampuni ya kutengeneza miwani ya jua ya "Melodies by MJB". Pia anafanya shughuli za matangazo na kampuni za Reebok, Air Jordan, Pepsi, Coca-Cola, Gap, Target, American Express, AT&T Inc., M∑A∑C, Apple Inc., Burger King na Chevrolet. Mwanamuziki huyo anaishi Saddle River, New Jersey, Marekani na anamiliki jumba lenye thamani ya Dola 17 milioni (Sh 26 bilioni). Pia ana magari kibao yakiwamo Chevloret, Royce Royce Phantom, Ferrari na Range Rover.
Popular Posts
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
BAADHI ya wananchi wa Ubungo katika Manispaa ya Kinondoni, jana wavamia Ofisi za Kampuni inayosambaza maji katika Jiji la Dar es Salaam na...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
Chimbuko la uvujaji wa mitihani nchini Tanzania lina historia ndefu inayoenda sambamba na kuundwa kwa BARAZA LA MITIHANI LA TAI...
-
RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni amewapandisha vyeo maofisa wa juu wa jeshi pamoja na kuwahamisha baadhi ya maofisa akiwemo mlinzi wake mk...
-
I: UTANGULIZI a) Masuala ya Jumla Mheshimiwa Spika, 1. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi M...
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK.Jakaya kikwete akilihutubia bunge mjini Dodoma.kulia ni spika wa Bunge Anne Makinda. Wab...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment