LOS ANGELES, Marekani MWANAMUZIKI Mary Jane Blige ni kati ya wanamuziki mahiri wa Marekani.Blige, aliyezaliwa Januari 11, 1971, pia anasifika kutokana na kuwa prodyuza na kucheza filamu. Ameshinda tuzo tisa za Grammy na American Music Award kutokana na muziki wa R&B, Rap, Gospel na Pop. Blige alianza muziki mwaka 1992 baada ya kutoa albamu ya kwanza aliyoipa jina la 'What's the 411'. Mwanamuziki huyo ameuza zaidi ya nakala milioni 50 za albamu za muziki sehemu mbalimbali duniani. Anahesabiwa kuwa miongoni mwa wanamuziki wa R&B wenye mafanikio zaidi katika kipindi cha miaka 25. Blige pia amejizolea sifa kubwa kutokana na kazi zake za filamu na manukato. Aling'ara katika filamu ya Tyler Perry iliyotolewa mwaka 2009. Mwanamuziki huyo anakadiriwa kuwa na utajiri wa kiasi cha Dola 45 milioni (Sh 70 bilioni). Mwaka 2004, alianzisha lebo ya Matriarch Records na amekuwa akisambaza kazi za wanamuziki mbalimbali. Pia anatengeneza manukato yanayoitwa My Life na My Life Blossom HSN. Blige pia ana kampuni ya kutengeneza miwani ya jua ya "Melodies by MJB". Pia anafanya shughuli za matangazo na kampuni za Reebok, Air Jordan, Pepsi, Coca-Cola, Gap, Target, American Express, AT&T Inc., M∑A∑C, Apple Inc., Burger King na Chevrolet. Mwanamuziki huyo anaishi Saddle River, New Jersey, Marekani na anamiliki jumba lenye thamani ya Dola 17 milioni (Sh 26 bilioni). Pia ana magari kibao yakiwamo Chevloret, Royce Royce Phantom, Ferrari na Range Rover.
Popular Posts
-
JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Cha...
-
Rais Dk.Kikwete akisimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wabena katika sherehe za kuzindua mkoa mpya ...
-
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya waombolezaji baada a kuwasili nyumbani kwa aliyekuwa Wazri wa Fedha, Dr. ...
-
MFUMUKO wa bei unaweza kuwakimbiza wawekezaji wanaotaka kuja nchini kuwekeza rasilimali zao kama utaendelea kukua kama ilivyo sasa.Kwa s...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), imezikutanisha kampuni za mafuta hapa nchini kwa lengo kuunda Bodi ya Wakurugenzi ya Kampu...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo jipya la K...
-
DHANA ya kwamba Tanzania tumekuwa hatufaidi maliasili zetu kama vile utalii, madini , pamoja na mlima Kilimanjaro, na badala yake fursa...
-
Ujerumani imerejesha mafuvu ya Wanambia ishirini waliofariki dunia baada ya fujo dhidi ya utawala wa ukoloni wa Kijerumani zaidi ya miaka 1...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment