LOS ANGELES, Marekani MWANAMUZIKI Mary Jane Blige ni kati ya wanamuziki mahiri wa Marekani.Blige, aliyezaliwa Januari 11, 1971, pia anasifika kutokana na kuwa prodyuza na kucheza filamu. Ameshinda tuzo tisa za Grammy na American Music Award kutokana na muziki wa R&B, Rap, Gospel na Pop. Blige alianza muziki mwaka 1992 baada ya kutoa albamu ya kwanza aliyoipa jina la 'What's the 411'. Mwanamuziki huyo ameuza zaidi ya nakala milioni 50 za albamu za muziki sehemu mbalimbali duniani. Anahesabiwa kuwa miongoni mwa wanamuziki wa R&B wenye mafanikio zaidi katika kipindi cha miaka 25. Blige pia amejizolea sifa kubwa kutokana na kazi zake za filamu na manukato. Aling'ara katika filamu ya Tyler Perry iliyotolewa mwaka 2009. Mwanamuziki huyo anakadiriwa kuwa na utajiri wa kiasi cha Dola 45 milioni (Sh 70 bilioni). Mwaka 2004, alianzisha lebo ya Matriarch Records na amekuwa akisambaza kazi za wanamuziki mbalimbali. Pia anatengeneza manukato yanayoitwa My Life na My Life Blossom HSN. Blige pia ana kampuni ya kutengeneza miwani ya jua ya "Melodies by MJB". Pia anafanya shughuli za matangazo na kampuni za Reebok, Air Jordan, Pepsi, Coca-Cola, Gap, Target, American Express, AT&T Inc., M∑A∑C, Apple Inc., Burger King na Chevrolet. Mwanamuziki huyo anaishi Saddle River, New Jersey, Marekani na anamiliki jumba lenye thamani ya Dola 17 milioni (Sh 26 bilioni). Pia ana magari kibao yakiwamo Chevloret, Royce Royce Phantom, Ferrari na Range Rover.
Popular Posts
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
KAMPUNI ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti imetoa msaada wa kilo 200 ...
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasafisha aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi ...
-
UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Maha...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment