LOS ANGELES, Marekani MWANAMUZIKI Mary Jane Blige ni kati ya wanamuziki mahiri wa Marekani.Blige, aliyezaliwa Januari 11, 1971, pia anasifika kutokana na kuwa prodyuza na kucheza filamu. Ameshinda tuzo tisa za Grammy na American Music Award kutokana na muziki wa R&B, Rap, Gospel na Pop. Blige alianza muziki mwaka 1992 baada ya kutoa albamu ya kwanza aliyoipa jina la 'What's the 411'. Mwanamuziki huyo ameuza zaidi ya nakala milioni 50 za albamu za muziki sehemu mbalimbali duniani. Anahesabiwa kuwa miongoni mwa wanamuziki wa R&B wenye mafanikio zaidi katika kipindi cha miaka 25. Blige pia amejizolea sifa kubwa kutokana na kazi zake za filamu na manukato. Aling'ara katika filamu ya Tyler Perry iliyotolewa mwaka 2009. Mwanamuziki huyo anakadiriwa kuwa na utajiri wa kiasi cha Dola 45 milioni (Sh 70 bilioni). Mwaka 2004, alianzisha lebo ya Matriarch Records na amekuwa akisambaza kazi za wanamuziki mbalimbali. Pia anatengeneza manukato yanayoitwa My Life na My Life Blossom HSN. Blige pia ana kampuni ya kutengeneza miwani ya jua ya "Melodies by MJB". Pia anafanya shughuli za matangazo na kampuni za Reebok, Air Jordan, Pepsi, Coca-Cola, Gap, Target, American Express, AT&T Inc., M∑A∑C, Apple Inc., Burger King na Chevrolet. Mwanamuziki huyo anaishi Saddle River, New Jersey, Marekani na anamiliki jumba lenye thamani ya Dola 17 milioni (Sh 26 bilioni). Pia ana magari kibao yakiwamo Chevloret, Royce Royce Phantom, Ferrari na Range Rover.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment