MWIGIZAJI Nyota katika tasnia ya filamu Swahiliwood, Yvonne Cherryl �Monalisa� amewashutumu wasanii wenzake kwa kusema uongo katika jamii kuhusu maisha yao halisi pamoja na malipo wanayopata. Binti huyo amedai kwa kufanya hivyo wasanii wengi wemejikuta katika maisha ya kuunga unga kutokana uongo huo. �Baadhi ya wasanii wa filamu wanadanganya sana kuhusu hali halisi ya maisha yao, mtu akipata nafasi ya kuongea na vyombo vya habari kuhusu malipo na maisha yake halisi utakuta akisema kuwa yeye bila kulipwa milioni tano hawezi kushiriki katika filamu, lakini ukweli hakuna msanii wa kawaida anayelipwa fedha kama hizo katika tasnia ya filamu Bongo mimi mwenyewe ni mtayarishaji,� anasema Monalisa. Anaendelea kudai kuwa kutokana na udanganyifu huo Serikali kupitia Bodi ya Filamu iliamua kuongeza gharama za kibali cha kurekodi filamu hadi kufikia Shilingi 500,000 jambo lilofanya wasanii walalamike kama ni fedha kubwa sana kulingana na malipo ya filamu, lakini ilitokana na udanganyifu kutoka kwa baadhi ya wasanii wa filamu kudanganya, mwanadada huyo anasema hali ya soko la filamu ni mbaya kwa sasa.
Popular Posts
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
RAIS Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo maofisa wakuu kutoka cheo cha Meja Jenerali kuwa Luteni Jenerali kuanzia Novemba 21,mwaka huu. K...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
-
Na Heka Paul na Shakila Galus- MAELEZO- Dar es salaam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuf...
-
MBUNGE wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu Sugu, ameungana na wananchi wanaotaka Katiba Mpya ifute uwepo wa wakuu wa wilaya...
-
Brazil's government has said it will implement 50bn reais ($30bn; £19bn) of spending cuts in order to curb inflation and help prevent t...
-
The rankings of Africa’s top higher education institutions is provided by the 4 International Colleges & Universities (4icu). ...
-
Katika Teknolojia Wiki Hii - Polisi yawasaka watumiaji Blackberry, wadukuzi walenga Blackberry, mashine za kupaa zilizotengenezwa nyumbani ...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment