HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msaada wa kuacha matumizi ya dawa za kulevya akipatiwa matibabu. Kwa mujibu wa The Kenyan Daily Post, mwanamuziki huyo alikubali kupatiwa matibabu na ni miongoni mwa watu kadhaa wanaopata matibabu ya kuachana na ulevi wa dawa hizo. Anasifika kwa uzuri, sauti nyororo na wepesi wa kuzungusha kiuno jukwaani. Lakini leo hii, mwanamuzi huyo anakabiliwa na tatizo na usugu wa matumizi ya dawa za kulevya. Ray C ambaye alianza kuimba akiwa na umri mdogo, alitumia utoto wake akiishi jijini Dar es Salaam na Uganda. Alianza kujulikana kama DJ wa redio jijini Dar es Salaam katika stesheni ya Clouds FM. Alipata mafunzo ya sauti na kuanza kuimba mpaka alipotoa albamu yake ya kwanza 'Mapenzi Yangu' mwaka 2003. Albamu ilifanya vizuri nchini Tanzania, lakini aliendelea na muziki na kuzindua albamu nyingine mwaka 2004 'Na Wewe Milele' iliyovuka mipaka ya Tanzania na kusambaa Afrika Mashariki. Baada ya kufanya vizuri katika albamu yake ya pili, Ray C alibahatika kushinda tuzo ya Kilimanjaro na Kisima Music Awards na kuchukua nafasi kati ya wanamuziki wanaofanya vema Afrika Mashariki. Alizindua albamu yake ya tatu iliyopewa jina la 'Ray C' mwaka 2007. Albamu hiyo ilikuwa na mchanganyiko wa taarab na bongo fleva. Mbali na kumudu mitindo hiyo ya muziki, Ray C ni mkali wa Bhangra, RnB lakini sasa makali yake hayo yote yameishia kwenye kliniki akipewa mbinu za kuachana na dawa za kulevya. Tangu kutolewa kwa picha za utupu za mwanamuziki huyo anayecheza na kuimba ndipo umaarufu wake ulipoathiriwa na kushuka kwa kasi. Ray C amewahi kufanya kazi za kimataifa pamoja na kuonekana katika mataifa ya Uingereza, Marekani, Ujerumani, Sweden, China, Uganda, Nigeria, India, Afrika Kusini na Kenya. Hivi karibuni msanii huyo aliweka makazi yake nchini Kenya na muziki wake umekuwa maarufu baada ya kufanya kolabo ya wimbo wake 'Moto moto' akimshirikisha staa 'French Boy'. Akiwa nchini Kenya aliendelea kupata matatizo mengi ikiwa ni pamoja na shutuma dhidi ya promota Sadat Muhindi na kuibuka kwa mzozo kati yake na mhariri nchini Kenya, Charles Otieno. Katika ugomvi wake na promota Saadat Muhindi kwamba alikuwa akimlazimisha kufanya naye mapenzi kabla ya kufanya shoo nchini Sudan, Ray C alipofanya mahojiano na Hot Secrets, aliweka nayana kuwa Saadat alianza kuchanganya biashara ya muziki na mapenzi. Kutokana na hilo, promota huyo aliamua kuahirisha ziara ya muziki ndani ya Kenya na Sudan, ziara ambayo ingechukua siku 10. Ray C alisema Muhindi alianza kuonyesha tamaa ya mapenzi dhidi yake wakati alipotua jijini Dar es Salaam kufanya utafiti wa kinywaji chake kipya kiitwacho Dash. Kinywaji hicho hakina kilevi. Akizungumzia tuhuma hizo Saadat alisema: �Kama anayoyasema yana ukweli wowote ilikuwa akaamua kuja tena Kenya baada ya mimi kuondoka Dar es Salaam? Lakini pia tujiulize kwanini alikuja na rafiki yake wa kiume huku akijua kuwa mimi ni mwovu na hakuwahi kumweleza hilo? �Kwa taarifa yako niliwalipia wote wawili tiketi za ndege kuja jijini Nairobi. Kama ningekuwa na nia mbaya kamwe nisingekuwa na akili ya wendawazimu kama hiyo. Naamini ulikuwa mpango wa kuniharibia biashara zangu.� Kabla ya dosari hiyo, Saadat alikubaliana na Ray C awe balozi wa kinywaji chake cha Dash nchini Tanzania na kuzunguka katika miji ipatayo 10 kutangaza kinywaji hicho. Lakini kilichotokea baadaye ni kuwa wakati walipofanya shoo mjini Nakuru, wawili hao wakatangaza kuvunjwa kwa mkataba.
Popular Posts
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
Pope Benedict XVI is in the Spanish capital, Madrid, for four days of events expected to be attended by hundreds of thousands of people. ...
-
Mkesha ulofanyika katika uwanja wa Taifa wa mpira katika kuliombea Taifa
-
Waziri wa Usalama wa Nchi, George Saitoti, alisema jeshi litawasaka wafuasi wa kikundi cha waislamu wenye siasa kali, al Shabaab, kokote wa...
-
Maandamano kupinga uroho wa makampuni yamefanywa sehemu mbali mbali za dunia, yakitiwa moyo na maandamano ya wiki mbili sasa yanayofanywa N...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
ALIYEKUWA Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi (DPA) wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Amatus Liyumba ambaye anatumikia kifungo cha miaka miwili je...
-
MWANASIASA machachari ambaye pia ni Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samuel Sitta ametangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Mu...
-
Mwanamfalme wa Uingereza Charles na mkewe Camilla, au The Prince of Wales and The Duchess of Cornwall, kama wanavyojulikana rasmi, watafany...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment