MTUNZI na mwigizaji wa filamu za Swahiliwood, Omary Clayton 'Ommy' ,amesisitiza kuwa yeye ndiye mwandishi wa filamu ya Shakira iliyoigizwa na kuandaliwa na mwigizaji nyota wa Bongo, Vincent Kigosi 'Ray'. Ommy ametamka hayo kufuatia utata uliojitokeza kuhusu filamu hiyo kwamba imeandikwa na Ali Yakuti. Ommy amedai kuwa muswada wa filamu ya Shakira alimkabidhi Ray ukiwa umekamilika kila kitu hivyo Ray badala ya kupokea yeye akamwambia ampatie Ali Yakuti aukague na kuruhusu utumike kwa sababu hadithi yake ilikuwa nzuri. �Ukweli mimi ndiye mwandishi wa muswada wa filamu ya Shakira, nakumbuka hata tulivyokutana katika mafunzo ya utayarishaji filamu na kaka Ali, alikiri kuwa mimi ndiye mwandishi," alisema. "Kukuthibitishia kuwa mimi ni mkali kuliko yeye, ulifanyika usaili na nilimpoteza vibaya hadi mimi kuchukuliwa na Wazungu. Kisanaa mimi bora kuliko yeye, kiumri yeye ni mkubwa, ninamheshimu ni kaka yangu." Mwanaspoti lilizungumza pia na Ali Yakuti naye alisema kuwa maneno ya mtunzi huyo amekuwa akiyasikia mara kwa mara, lakini kwa sababu ukweli upo wazi hana sababu ya kubishana na mtu anayetafuta umaarufu kupitia kazi za watu wengine. "Ommy alikuja na kusimulia wazo ambalo halikuwa limekamilika. Mimi ndiye niliyeandika muswada," alisema Yakuti.
Popular Posts
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
KAMPUNI ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti imetoa msaada wa kilo 200 ...
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasafisha aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi ...
-
UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Maha...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment