MTUNZI na mwigizaji wa filamu za Swahiliwood, Omary Clayton 'Ommy' ,amesisitiza kuwa yeye ndiye mwandishi wa filamu ya Shakira iliyoigizwa na kuandaliwa na mwigizaji nyota wa Bongo, Vincent Kigosi 'Ray'. Ommy ametamka hayo kufuatia utata uliojitokeza kuhusu filamu hiyo kwamba imeandikwa na Ali Yakuti. Ommy amedai kuwa muswada wa filamu ya Shakira alimkabidhi Ray ukiwa umekamilika kila kitu hivyo Ray badala ya kupokea yeye akamwambia ampatie Ali Yakuti aukague na kuruhusu utumike kwa sababu hadithi yake ilikuwa nzuri. �Ukweli mimi ndiye mwandishi wa muswada wa filamu ya Shakira, nakumbuka hata tulivyokutana katika mafunzo ya utayarishaji filamu na kaka Ali, alikiri kuwa mimi ndiye mwandishi," alisema. "Kukuthibitishia kuwa mimi ni mkali kuliko yeye, ulifanyika usaili na nilimpoteza vibaya hadi mimi kuchukuliwa na Wazungu. Kisanaa mimi bora kuliko yeye, kiumri yeye ni mkubwa, ninamheshimu ni kaka yangu." Mwanaspoti lilizungumza pia na Ali Yakuti naye alisema kuwa maneno ya mtunzi huyo amekuwa akiyasikia mara kwa mara, lakini kwa sababu ukweli upo wazi hana sababu ya kubishana na mtu anayetafuta umaarufu kupitia kazi za watu wengine. "Ommy alikuja na kusimulia wazo ambalo halikuwa limekamilika. Mimi ndiye niliyeandika muswada," alisema Yakuti.
Popular Posts
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
BAADHI ya wananchi wa Ubungo katika Manispaa ya Kinondoni, jana wavamia Ofisi za Kampuni inayosambaza maji katika Jiji la Dar es Salaam na...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
Chimbuko la uvujaji wa mitihani nchini Tanzania lina historia ndefu inayoenda sambamba na kuundwa kwa BARAZA LA MITIHANI LA TAI...
-
RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni amewapandisha vyeo maofisa wa juu wa jeshi pamoja na kuwahamisha baadhi ya maofisa akiwemo mlinzi wake mk...
-
I: UTANGULIZI a) Masuala ya Jumla Mheshimiwa Spika, 1. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi M...
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK.Jakaya kikwete akilihutubia bunge mjini Dodoma.kulia ni spika wa Bunge Anne Makinda. Wab...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment