MTUNZI na mwigizaji wa filamu za Swahiliwood, Omary Clayton 'Ommy' ,amesisitiza kuwa yeye ndiye mwandishi wa filamu ya Shakira iliyoigizwa na kuandaliwa na mwigizaji nyota wa Bongo, Vincent Kigosi 'Ray'. Ommy ametamka hayo kufuatia utata uliojitokeza kuhusu filamu hiyo kwamba imeandikwa na Ali Yakuti. Ommy amedai kuwa muswada wa filamu ya Shakira alimkabidhi Ray ukiwa umekamilika kila kitu hivyo Ray badala ya kupokea yeye akamwambia ampatie Ali Yakuti aukague na kuruhusu utumike kwa sababu hadithi yake ilikuwa nzuri. �Ukweli mimi ndiye mwandishi wa muswada wa filamu ya Shakira, nakumbuka hata tulivyokutana katika mafunzo ya utayarishaji filamu na kaka Ali, alikiri kuwa mimi ndiye mwandishi," alisema. "Kukuthibitishia kuwa mimi ni mkali kuliko yeye, ulifanyika usaili na nilimpoteza vibaya hadi mimi kuchukuliwa na Wazungu. Kisanaa mimi bora kuliko yeye, kiumri yeye ni mkubwa, ninamheshimu ni kaka yangu." Mwanaspoti lilizungumza pia na Ali Yakuti naye alisema kuwa maneno ya mtunzi huyo amekuwa akiyasikia mara kwa mara, lakini kwa sababu ukweli upo wazi hana sababu ya kubishana na mtu anayetafuta umaarufu kupitia kazi za watu wengine. "Ommy alikuja na kusimulia wazo ambalo halikuwa limekamilika. Mimi ndiye niliyeandika muswada," alisema Yakuti.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment