MTUNZI na mwigizaji wa filamu za Swahiliwood, Omary Clayton 'Ommy' ,amesisitiza kuwa yeye ndiye mwandishi wa filamu ya Shakira iliyoigizwa na kuandaliwa na mwigizaji nyota wa Bongo, Vincent Kigosi 'Ray'. Ommy ametamka hayo kufuatia utata uliojitokeza kuhusu filamu hiyo kwamba imeandikwa na Ali Yakuti. Ommy amedai kuwa muswada wa filamu ya Shakira alimkabidhi Ray ukiwa umekamilika kila kitu hivyo Ray badala ya kupokea yeye akamwambia ampatie Ali Yakuti aukague na kuruhusu utumike kwa sababu hadithi yake ilikuwa nzuri. �Ukweli mimi ndiye mwandishi wa muswada wa filamu ya Shakira, nakumbuka hata tulivyokutana katika mafunzo ya utayarishaji filamu na kaka Ali, alikiri kuwa mimi ndiye mwandishi," alisema. "Kukuthibitishia kuwa mimi ni mkali kuliko yeye, ulifanyika usaili na nilimpoteza vibaya hadi mimi kuchukuliwa na Wazungu. Kisanaa mimi bora kuliko yeye, kiumri yeye ni mkubwa, ninamheshimu ni kaka yangu." Mwanaspoti lilizungumza pia na Ali Yakuti naye alisema kuwa maneno ya mtunzi huyo amekuwa akiyasikia mara kwa mara, lakini kwa sababu ukweli upo wazi hana sababu ya kubishana na mtu anayetafuta umaarufu kupitia kazi za watu wengine. "Ommy alikuja na kusimulia wazo ambalo halikuwa limekamilika. Mimi ndiye niliyeandika muswada," alisema Yakuti.
Popular Posts
-
JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Cha...
-
Rais Dk.Kikwete akisimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wabena katika sherehe za kuzindua mkoa mpya ...
-
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya waombolezaji baada a kuwasili nyumbani kwa aliyekuwa Wazri wa Fedha, Dr. ...
-
MFUMUKO wa bei unaweza kuwakimbiza wawekezaji wanaotaka kuja nchini kuwekeza rasilimali zao kama utaendelea kukua kama ilivyo sasa.Kwa s...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), imezikutanisha kampuni za mafuta hapa nchini kwa lengo kuunda Bodi ya Wakurugenzi ya Kampu...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo jipya la K...
-
DHANA ya kwamba Tanzania tumekuwa hatufaidi maliasili zetu kama vile utalii, madini , pamoja na mlima Kilimanjaro, na badala yake fursa...
-
Ujerumani imerejesha mafuvu ya Wanambia ishirini waliofariki dunia baada ya fujo dhidi ya utawala wa ukoloni wa Kijerumani zaidi ya miaka 1...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment