WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo imekuja siku kadhaa baada ya baadhi ya vyombo vya habari, kutangaza kuwepo kwa mgao wa umeme nchini. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, alisema mgao ulijitokeza za katika Mkoa wa Dar es Salaam, ulisababishwa na kuungua kwa transfoma mbili zenye ukubwa wa 15 MVA na Kv 33/11 zilizopo katikati ya Jiji. Alisema tatizo hilo lilianza Machi 6 mwaka huu ambapo umeme ulikatika kutokana na hitilafu katika kituo cha kupoozea umeme ilichoko mkabala na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Maswi alisema baada ya hitilafu hiyo, Serikali iliamua kugharamia manunuzi ya ya transfoma nne zenye thamani ya Dola 350 milioni kwa utaratibu wa dharura. Kuhusu deni la Tanesco la Sh 279 bilioni, alisema deni hilo si la kweli na kwamba deni halisi ni Sh 79 bilion. “Deni tunalodaiwa ni Sh 79 bilioni lakini wao wamejulisha hadi madeni ya miradi ambayo imeingia mikataba na shirika pamoja na makampuni ambazo zinafanya kazi na shirika letu,”alisema na kuongeza Katika hatua nyingine, wizara ipo katika mkakati wa kuongeza megawati 100 za umeme ili kufikia megawati 1370 Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanesco, William Mhando, alisema baada ya kupata Sh 408 bilioni shirika linajipanga kubadilisha miundombinu yake.
Popular Posts
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
KAMPUNI ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti imetoa msaada wa kilo 200 ...
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasafisha aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi ...
-
UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Maha...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment