WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo imekuja siku kadhaa baada ya baadhi ya vyombo vya habari, kutangaza kuwepo kwa mgao wa umeme nchini. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, alisema mgao ulijitokeza za katika Mkoa wa Dar es Salaam, ulisababishwa na kuungua kwa transfoma mbili zenye ukubwa wa 15 MVA na Kv 33/11 zilizopo katikati ya Jiji. Alisema tatizo hilo lilianza Machi 6 mwaka huu ambapo umeme ulikatika kutokana na hitilafu katika kituo cha kupoozea umeme ilichoko mkabala na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Maswi alisema baada ya hitilafu hiyo, Serikali iliamua kugharamia manunuzi ya ya transfoma nne zenye thamani ya Dola 350 milioni kwa utaratibu wa dharura. Kuhusu deni la Tanesco la Sh 279 bilioni, alisema deni hilo si la kweli na kwamba deni halisi ni Sh 79 bilion. “Deni tunalodaiwa ni Sh 79 bilioni lakini wao wamejulisha hadi madeni ya miradi ambayo imeingia mikataba na shirika pamoja na makampuni ambazo zinafanya kazi na shirika letu,”alisema na kuongeza Katika hatua nyingine, wizara ipo katika mkakati wa kuongeza megawati 100 za umeme ili kufikia megawati 1370 Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanesco, William Mhando, alisema baada ya kupata Sh 408 bilioni shirika linajipanga kubadilisha miundombinu yake.
Popular Posts
-
JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Cha...
-
Rais Dk.Kikwete akisimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wabena katika sherehe za kuzindua mkoa mpya ...
-
NEEMA imeendelea kumdondokea mwanamuziki Chaz Baba ambaye baada ya kuhamia Bendi ya Mashujaa Musica na kuvuta mkwanja mrefu, sasa amechag...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali mtoto Andrew Simba(15) aliyelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wakati Rais alipowate...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), imezikutanisha kampuni za mafuta hapa nchini kwa lengo kuunda Bodi ya Wakurugenzi ya Kampu...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
Mwanaharakati wa haki za binadamu nchini Kenya Al-Amin Kimathi ni miogoni mwa washukiwa watano wa shambulio la bomu la mjini Kampala wakati...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment