WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo imekuja siku kadhaa baada ya baadhi ya vyombo vya habari, kutangaza kuwepo kwa mgao wa umeme nchini. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, alisema mgao ulijitokeza za katika Mkoa wa Dar es Salaam, ulisababishwa na kuungua kwa transfoma mbili zenye ukubwa wa 15 MVA na Kv 33/11 zilizopo katikati ya Jiji. Alisema tatizo hilo lilianza Machi 6 mwaka huu ambapo umeme ulikatika kutokana na hitilafu katika kituo cha kupoozea umeme ilichoko mkabala na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Maswi alisema baada ya hitilafu hiyo, Serikali iliamua kugharamia manunuzi ya ya transfoma nne zenye thamani ya Dola 350 milioni kwa utaratibu wa dharura. Kuhusu deni la Tanesco la Sh 279 bilioni, alisema deni hilo si la kweli na kwamba deni halisi ni Sh 79 bilion. “Deni tunalodaiwa ni Sh 79 bilioni lakini wao wamejulisha hadi madeni ya miradi ambayo imeingia mikataba na shirika pamoja na makampuni ambazo zinafanya kazi na shirika letu,”alisema na kuongeza Katika hatua nyingine, wizara ipo katika mkakati wa kuongeza megawati 100 za umeme ili kufikia megawati 1370 Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Tanesco, William Mhando, alisema baada ya kupata Sh 408 bilioni shirika linajipanga kubadilisha miundombinu yake.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni amewapandisha vyeo maofisa wa juu wa jeshi pamoja na kuwahamisha baadhi ya maofisa akiwemo mlinzi wake mk...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment