NEEMA imeendelea kumdondokea mwanamuziki Chaz Baba ambaye baada ya kuhamia Bendi ya Mashujaa Musica na kuvuta mkwanja mrefu, sasa amechaguliwa kuwa rais wa bendi hiyo. Kuchaguliwa kuwa rais wa bendi, maana yake ni kuwa mfuko utazidi kutuna kwa kuwa cheo hicho ni lazima kiendane sambamba na marupurupu. Akizungumza na gazeti hili Mkurugenzi wa bendi hiyo, Max Luhanga amesema, kwa kuwa majukumu ya Chaz Baba yameongezeka ni wazi kuwa marupurupu yataongezeka ingawa mpaka sasa bado hawajaamua ni kwa kiasi gani watamuongezea mshiko. "Hivi sasa Chaz atakuwa na kazi nyingi, lakini hadhi ya cheo ni lazima iendane na mapato, huwezi kumwita rais halafu akawa choka mbaya, lengo letu ni kuboresha maisha ya wanamuziki wetu pia," anasema Max. Chaz Baba aliibuka kidedea kwa kura 19 dhidi ya 26 zilizopigwa na kuwabwaga wanamuziki wenzake Sauti ya Radi na Mirinda Nyeusi. Rais Chaz Baba anachukua nafasi hiyo iliyokuwa inashikiliwa na mwanamuziki mwenzake anayefahamika kwa jina moja la Kajo. Hata hivyo kuingia madarakani kwa Chaz Baba pia kumemsababishia rais wa zamani, Kajo kutimuliwa kwa kundini kwa kile ambacho mkurugenzi anasema ni utovu wa nidhamu. Max anasema baada ya Chaz Baba kuchaguliwa, Kajo aligoma kutoa ushirikiano kwa rais mpya ikiwemo kumkabidhi ofisi. Mbali na kuwa katika safu ya mbele ya uimbaji, Chaz Baba sasa anakuwa na majukumu ya kupanga programu za shoo, kupanga mavazi ya wanamuziki, kusikiliza na kusimamia maoni, ushauri na kutatua matatizo ya wanamuziki. Bendi hiyo inaongozwa na Mkurugenzi, Max Luhanga, Meneja, King Dodoo na Rais ni Chaz Baba kuanzia Machi 27.
Popular Posts
-
JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Cha...
-
Rais Dk.Kikwete akisimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wabena katika sherehe za kuzindua mkoa mpya ...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
NEEMA imeendelea kumdondokea mwanamuziki Chaz Baba ambaye baada ya kuhamia Bendi ya Mashujaa Musica na kuvuta mkwanja mrefu, sasa amechag...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Mwanaharakati wa haki za binadamu nchini Kenya Al-Amin Kimathi ni miogoni mwa washukiwa watano wa shambulio la bomu la mjini Kampala wakati...
-
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itafanya kila juhudi kuhakikisha...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo jipya la K...
-
DHANA ya kwamba Tanzania tumekuwa hatufaidi maliasili zetu kama vile utalii, madini , pamoja na mlima Kilimanjaro, na badala yake fursa...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment