NEEMA imeendelea kumdondokea mwanamuziki Chaz Baba ambaye baada ya kuhamia Bendi ya Mashujaa Musica na kuvuta mkwanja mrefu, sasa amechaguliwa kuwa rais wa bendi hiyo. Kuchaguliwa kuwa rais wa bendi, maana yake ni kuwa mfuko utazidi kutuna kwa kuwa cheo hicho ni lazima kiendane sambamba na marupurupu. Akizungumza na gazeti hili Mkurugenzi wa bendi hiyo, Max Luhanga amesema, kwa kuwa majukumu ya Chaz Baba yameongezeka ni wazi kuwa marupurupu yataongezeka ingawa mpaka sasa bado hawajaamua ni kwa kiasi gani watamuongezea mshiko. "Hivi sasa Chaz atakuwa na kazi nyingi, lakini hadhi ya cheo ni lazima iendane na mapato, huwezi kumwita rais halafu akawa choka mbaya, lengo letu ni kuboresha maisha ya wanamuziki wetu pia," anasema Max. Chaz Baba aliibuka kidedea kwa kura 19 dhidi ya 26 zilizopigwa na kuwabwaga wanamuziki wenzake Sauti ya Radi na Mirinda Nyeusi. Rais Chaz Baba anachukua nafasi hiyo iliyokuwa inashikiliwa na mwanamuziki mwenzake anayefahamika kwa jina moja la Kajo. Hata hivyo kuingia madarakani kwa Chaz Baba pia kumemsababishia rais wa zamani, Kajo kutimuliwa kwa kundini kwa kile ambacho mkurugenzi anasema ni utovu wa nidhamu. Max anasema baada ya Chaz Baba kuchaguliwa, Kajo aligoma kutoa ushirikiano kwa rais mpya ikiwemo kumkabidhi ofisi. Mbali na kuwa katika safu ya mbele ya uimbaji, Chaz Baba sasa anakuwa na majukumu ya kupanga programu za shoo, kupanga mavazi ya wanamuziki, kusikiliza na kusimamia maoni, ushauri na kutatua matatizo ya wanamuziki. Bendi hiyo inaongozwa na Mkurugenzi, Max Luhanga, Meneja, King Dodoo na Rais ni Chaz Baba kuanzia Machi 27.
Popular Posts
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
Pope Benedict XVI is in the Spanish capital, Madrid, for four days of events expected to be attended by hundreds of thousands of people. ...
-
Mkesha ulofanyika katika uwanja wa Taifa wa mpira katika kuliombea Taifa
-
Waziri wa Usalama wa Nchi, George Saitoti, alisema jeshi litawasaka wafuasi wa kikundi cha waislamu wenye siasa kali, al Shabaab, kokote wa...
-
Maandamano kupinga uroho wa makampuni yamefanywa sehemu mbali mbali za dunia, yakitiwa moyo na maandamano ya wiki mbili sasa yanayofanywa N...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
ALIYEKUWA Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi (DPA) wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Amatus Liyumba ambaye anatumikia kifungo cha miaka miwili je...
-
MWANASIASA machachari ambaye pia ni Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samuel Sitta ametangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Mu...
-
Mwanamfalme wa Uingereza Charles na mkewe Camilla, au The Prince of Wales and The Duchess of Cornwall, kama wanavyojulikana rasmi, watafany...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment