NEEMA imeendelea kumdondokea mwanamuziki Chaz Baba ambaye baada ya kuhamia Bendi ya Mashujaa Musica na kuvuta mkwanja mrefu, sasa amechaguliwa kuwa rais wa bendi hiyo. Kuchaguliwa kuwa rais wa bendi, maana yake ni kuwa mfuko utazidi kutuna kwa kuwa cheo hicho ni lazima kiendane sambamba na marupurupu. Akizungumza na gazeti hili Mkurugenzi wa bendi hiyo, Max Luhanga amesema, kwa kuwa majukumu ya Chaz Baba yameongezeka ni wazi kuwa marupurupu yataongezeka ingawa mpaka sasa bado hawajaamua ni kwa kiasi gani watamuongezea mshiko. "Hivi sasa Chaz atakuwa na kazi nyingi, lakini hadhi ya cheo ni lazima iendane na mapato, huwezi kumwita rais halafu akawa choka mbaya, lengo letu ni kuboresha maisha ya wanamuziki wetu pia," anasema Max. Chaz Baba aliibuka kidedea kwa kura 19 dhidi ya 26 zilizopigwa na kuwabwaga wanamuziki wenzake Sauti ya Radi na Mirinda Nyeusi. Rais Chaz Baba anachukua nafasi hiyo iliyokuwa inashikiliwa na mwanamuziki mwenzake anayefahamika kwa jina moja la Kajo. Hata hivyo kuingia madarakani kwa Chaz Baba pia kumemsababishia rais wa zamani, Kajo kutimuliwa kwa kundini kwa kile ambacho mkurugenzi anasema ni utovu wa nidhamu. Max anasema baada ya Chaz Baba kuchaguliwa, Kajo aligoma kutoa ushirikiano kwa rais mpya ikiwemo kumkabidhi ofisi. Mbali na kuwa katika safu ya mbele ya uimbaji, Chaz Baba sasa anakuwa na majukumu ya kupanga programu za shoo, kupanga mavazi ya wanamuziki, kusikiliza na kusimamia maoni, ushauri na kutatua matatizo ya wanamuziki. Bendi hiyo inaongozwa na Mkurugenzi, Max Luhanga, Meneja, King Dodoo na Rais ni Chaz Baba kuanzia Machi 27.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment