NEEMA imeendelea kumdondokea mwanamuziki Chaz Baba ambaye baada ya kuhamia Bendi ya Mashujaa Musica na kuvuta mkwanja mrefu, sasa amechaguliwa kuwa rais wa bendi hiyo. Kuchaguliwa kuwa rais wa bendi, maana yake ni kuwa mfuko utazidi kutuna kwa kuwa cheo hicho ni lazima kiendane sambamba na marupurupu. Akizungumza na gazeti hili Mkurugenzi wa bendi hiyo, Max Luhanga amesema, kwa kuwa majukumu ya Chaz Baba yameongezeka ni wazi kuwa marupurupu yataongezeka ingawa mpaka sasa bado hawajaamua ni kwa kiasi gani watamuongezea mshiko. "Hivi sasa Chaz atakuwa na kazi nyingi, lakini hadhi ya cheo ni lazima iendane na mapato, huwezi kumwita rais halafu akawa choka mbaya, lengo letu ni kuboresha maisha ya wanamuziki wetu pia," anasema Max. Chaz Baba aliibuka kidedea kwa kura 19 dhidi ya 26 zilizopigwa na kuwabwaga wanamuziki wenzake Sauti ya Radi na Mirinda Nyeusi. Rais Chaz Baba anachukua nafasi hiyo iliyokuwa inashikiliwa na mwanamuziki mwenzake anayefahamika kwa jina moja la Kajo. Hata hivyo kuingia madarakani kwa Chaz Baba pia kumemsababishia rais wa zamani, Kajo kutimuliwa kwa kundini kwa kile ambacho mkurugenzi anasema ni utovu wa nidhamu. Max anasema baada ya Chaz Baba kuchaguliwa, Kajo aligoma kutoa ushirikiano kwa rais mpya ikiwemo kumkabidhi ofisi. Mbali na kuwa katika safu ya mbele ya uimbaji, Chaz Baba sasa anakuwa na majukumu ya kupanga programu za shoo, kupanga mavazi ya wanamuziki, kusikiliza na kusimamia maoni, ushauri na kutatua matatizo ya wanamuziki. Bendi hiyo inaongozwa na Mkurugenzi, Max Luhanga, Meneja, King Dodoo na Rais ni Chaz Baba kuanzia Machi 27.
Popular Posts
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
KAMPUNI ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti imetoa msaada wa kilo 200 ...
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasafisha aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi ...
-
UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Maha...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment