MFUMUKO wa bei unaweza kuwakimbiza wawekezaji wanaotaka kuja nchini kuwekeza rasilimali zao kama utaendelea kukua kama ilivyo sasa.Kwa sasa kiwango cha mfumuko wa bei, kimefikia asilimia 19. Tahadhari hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered, Jeremy Awori, alipokuwa akiwasilisha mada yake katika semina ya Mameneja wa Rasilimali Watu kutoka kampuni mbalimbali. Semina hiyo iliyokuwa na lengo la kuangalia masuala mbalimbali ya rasilimali watu iliandaliwa na Chama cha Wanataaluma ya Rasilimali Watu Tanzania. Awori alisema tafiti zinaonyesha kuwa Tanzania ndiyo yenye mfumuko mkubwa wa bei miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki, jambo linaloweza kuathiri biasharana za uwekezaji.“Mfumuko wa bei ukiwa juu mwekezaji analinganisha na nchi nyingine akiona kule hakuna mfumuko mkubwa anajiuliza kwanini niwekeze hapa ambapo itanigharimu sana wakati kuna nchi mfumuko uko chini na anaweza kufanyabiashara vizuri, maana mfumuko wa bei unasababisha gharama kubwa hata unapoajiri watu,” alisema. Pia alisema Tanzania ina fursa ya kukuza uchumi wake kwa kiwango kikubwa hasa ikizingatiwa kuwa imejaliwa kuwa na rasilimali nyingi kuliko nchi nyingi za Afrika.Alisema Tanzania ina madini mengi na maliasili nyingi ambazo hazipatikani katika nchi nyingi na kwamba hiyo ni fursa kubwa ya kuwezesha uchumi kupaa kwa haraka. “Kuna vitu vingine huhitaji kuambiwa, hivi nani asiyejua kuwa Tanzania imejaa madini na maliasili za kutosha, tukivitumia hivi vizuri inaweza kuwa njia ya kutosha kuondokana na hali iliyopo sasa,” alisisitiza.Awori alisema biashara kati ya Tanzania na mataifa makubwa kama China, inaongezeka na kwamba kuna haja kwa wanataaluma kuichukua hiyo kama fursa kwao. Alitoa mfano kuwa Wachina wengi wanakuja Tanzania kuendesha miradi mikubwa katika sekta mbalimbali kama ujenzi na kwamba wanahitaji huduma mbalimbali kama za kibenki.
Popular Posts
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
KAMPUNI ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti imetoa msaada wa kilo 200 ...
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasafisha aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi ...
-
UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Maha...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment