MFUMUKO wa bei unaweza kuwakimbiza wawekezaji wanaotaka kuja nchini kuwekeza rasilimali zao kama utaendelea kukua kama ilivyo sasa.Kwa sasa kiwango cha mfumuko wa bei, kimefikia asilimia 19. Tahadhari hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered, Jeremy Awori, alipokuwa akiwasilisha mada yake katika semina ya Mameneja wa Rasilimali Watu kutoka kampuni mbalimbali. Semina hiyo iliyokuwa na lengo la kuangalia masuala mbalimbali ya rasilimali watu iliandaliwa na Chama cha Wanataaluma ya Rasilimali Watu Tanzania. Awori alisema tafiti zinaonyesha kuwa Tanzania ndiyo yenye mfumuko mkubwa wa bei miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki, jambo linaloweza kuathiri biasharana za uwekezaji.“Mfumuko wa bei ukiwa juu mwekezaji analinganisha na nchi nyingine akiona kule hakuna mfumuko mkubwa anajiuliza kwanini niwekeze hapa ambapo itanigharimu sana wakati kuna nchi mfumuko uko chini na anaweza kufanyabiashara vizuri, maana mfumuko wa bei unasababisha gharama kubwa hata unapoajiri watu,” alisema. Pia alisema Tanzania ina fursa ya kukuza uchumi wake kwa kiwango kikubwa hasa ikizingatiwa kuwa imejaliwa kuwa na rasilimali nyingi kuliko nchi nyingi za Afrika.Alisema Tanzania ina madini mengi na maliasili nyingi ambazo hazipatikani katika nchi nyingi na kwamba hiyo ni fursa kubwa ya kuwezesha uchumi kupaa kwa haraka. “Kuna vitu vingine huhitaji kuambiwa, hivi nani asiyejua kuwa Tanzania imejaa madini na maliasili za kutosha, tukivitumia hivi vizuri inaweza kuwa njia ya kutosha kuondokana na hali iliyopo sasa,” alisisitiza.Awori alisema biashara kati ya Tanzania na mataifa makubwa kama China, inaongezeka na kwamba kuna haja kwa wanataaluma kuichukua hiyo kama fursa kwao. Alitoa mfano kuwa Wachina wengi wanakuja Tanzania kuendesha miradi mikubwa katika sekta mbalimbali kama ujenzi na kwamba wanahitaji huduma mbalimbali kama za kibenki.
Popular Posts
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
BAADHI ya wananchi wa Ubungo katika Manispaa ya Kinondoni, jana wavamia Ofisi za Kampuni inayosambaza maji katika Jiji la Dar es Salaam na...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
Chimbuko la uvujaji wa mitihani nchini Tanzania lina historia ndefu inayoenda sambamba na kuundwa kwa BARAZA LA MITIHANI LA TAI...
-
RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni amewapandisha vyeo maofisa wa juu wa jeshi pamoja na kuwahamisha baadhi ya maofisa akiwemo mlinzi wake mk...
-
I: UTANGULIZI a) Masuala ya Jumla Mheshimiwa Spika, 1. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi M...
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK.Jakaya kikwete akilihutubia bunge mjini Dodoma.kulia ni spika wa Bunge Anne Makinda. Wab...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment