MFUMUKO wa bei unaweza kuwakimbiza wawekezaji wanaotaka kuja nchini kuwekeza rasilimali zao kama utaendelea kukua kama ilivyo sasa.Kwa sasa kiwango cha mfumuko wa bei, kimefikia asilimia 19. Tahadhari hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Benki ya Standard Chartered, Jeremy Awori, alipokuwa akiwasilisha mada yake katika semina ya Mameneja wa Rasilimali Watu kutoka kampuni mbalimbali. Semina hiyo iliyokuwa na lengo la kuangalia masuala mbalimbali ya rasilimali watu iliandaliwa na Chama cha Wanataaluma ya Rasilimali Watu Tanzania. Awori alisema tafiti zinaonyesha kuwa Tanzania ndiyo yenye mfumuko mkubwa wa bei miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki, jambo linaloweza kuathiri biasharana za uwekezaji.“Mfumuko wa bei ukiwa juu mwekezaji analinganisha na nchi nyingine akiona kule hakuna mfumuko mkubwa anajiuliza kwanini niwekeze hapa ambapo itanigharimu sana wakati kuna nchi mfumuko uko chini na anaweza kufanyabiashara vizuri, maana mfumuko wa bei unasababisha gharama kubwa hata unapoajiri watu,” alisema. Pia alisema Tanzania ina fursa ya kukuza uchumi wake kwa kiwango kikubwa hasa ikizingatiwa kuwa imejaliwa kuwa na rasilimali nyingi kuliko nchi nyingi za Afrika.Alisema Tanzania ina madini mengi na maliasili nyingi ambazo hazipatikani katika nchi nyingi na kwamba hiyo ni fursa kubwa ya kuwezesha uchumi kupaa kwa haraka. “Kuna vitu vingine huhitaji kuambiwa, hivi nani asiyejua kuwa Tanzania imejaa madini na maliasili za kutosha, tukivitumia hivi vizuri inaweza kuwa njia ya kutosha kuondokana na hali iliyopo sasa,” alisisitiza.Awori alisema biashara kati ya Tanzania na mataifa makubwa kama China, inaongezeka na kwamba kuna haja kwa wanataaluma kuichukua hiyo kama fursa kwao. Alitoa mfano kuwa Wachina wengi wanakuja Tanzania kuendesha miradi mikubwa katika sekta mbalimbali kama ujenzi na kwamba wanahitaji huduma mbalimbali kama za kibenki.
Popular Posts
-
I: UTANGULIZI a) Masuala ya Jumla Mheshimiwa Spika, 1. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi M...
-
Mtaalamu kutoka Finland asaidia mikakati ya tehama
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bunge ya Hesbu za Mashirika ya Umma, Kabwe Zuberi Zitto, akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma ...
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
JOSEPH KABILA Ni kijana na anawakilisha mustakabali wa nchi," Ndivyo walivyosema wafuasi wa Joseph Kabila wakati akiwasilisha fomu ...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment