VILIO na simanzi kubwa, jana viligubika katika mazishi ya mtoto mdogo, Teneli Malemi
Mang’ombe (11), aliyeuawa kwa kupigwa risasi na mwenyekiti wa zamani wa CCM Mkoa wa
Mwanza, Clement Mabina.
Mazishi hayo yalifanyika nyumbani kwa marehemu Kitongoji cha Kanyama, Kata ya Kisesa
wilayani Magu mkoani hapa.
Katika ibada ya mazishi hayo iliyoongozwa na Paroko wa Parokia ya Bujora Kisesa, Padri
Fabian Mhoja, akisaidiwa na Katekista wa Parokia hiyo, Faustine Lucas, ilihudhuriwa na
viongozi mbalimbali wa CCM na CHADEMA na serikali wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya
Magu, Jacqueline Liana.
CCM washukuru kutotimuliwa msibani
Akitoa salamu za chama mara baada ya kumalizika maziko ya mtoto huyo aliyekuwa akisoma
darasa la sita Shule ya Msingi Kanyama, Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Joyce Masunga
alisema: “Tulishtushwa sana tuliposikia tukio hili. Lakini tunashukuru wazazi, ndugu na jamaa
hamjatufukuza kwenye msiba huu.”
Katibu huyo mbali na kutotoa rambirambi ya fedha, alijivunia chama chake kuandaa chakula
msibani hapo, na yeye kuosha mwili wa marehemu Taneli kwenye chumba cha kuhifadhia
marehemu hospitali ya Bugando.
“Kwa niaba ya chama tawala cha CCM, ninashukuru sana familia ya marehemu maana
hamjatufukuza katika msiba huu. Ingekuwa sehemu nyingine tungeweza kufukuzwa kwa sababu
kiongozi wa CCM amehusika kuua. Ila naomba sana tuweni na upendo, uvumilivu na amani,”
alisema Masunga huku akipiga magoti.
Mkuu wa wilaya hiyo, Jacqueline Liana alisema: “Kila mtu asimamie amani. Tukio kama hili
lisitokee tena katika wilaya yangu hii ya Magu, na ikiwezekana liwe la kwanza na la mwisho
kote nchini. Na Serikali ya Magu inatoa pole ya rambirambi kwa familia ya marehemu ya sh
300,000.”
Taneli aliuawa kwa kupigwa risasi na Mabina kisha nae kuuawa na wananchi papo hapo,
Desemba 15 mwaka huu, katika ugomvi wa mashamba kati yake na wananchi wa Kanyama.
Mazishi ya Mabina yawa gumzo
Wakati huo huo, Mabina ambaye alikuwa diwani wa Kata ya Kisesa wilayani Magu na mjumbe
wa mkutano mkuu wa taifa CCM aliyeuawa na wananchi wenye hasira, anatarajiwa kuzikwa
kesho, ambapo mazishi yake yatagharimu sh milioni 22.
Tetesi zilizopatikana kutoka kwa baadhi ya waombolezaji nyumbani kwa marehemu Mabina,
zinaeleza kwamba, Rais Jakaya Kikwete huenda akaongoza mazishi ya kiongozi huyo.
Baadhi ya wananchi wa Kisesa walionekana kufurahi kuuawa kwa kiongozi huyo, kwa madai
kwamba alikuwa amewasumbua kwa kuwadhulumu mashamba kwa muda mrefu.
MABINA AZIKWA KESHO
Jitokezedirectory
Thursday, December 19, 2013
Popular Posts
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
Pope Benedict XVI is in the Spanish capital, Madrid, for four days of events expected to be attended by hundreds of thousands of people. ...
-
Mkesha ulofanyika katika uwanja wa Taifa wa mpira katika kuliombea Taifa
-
Waziri wa Usalama wa Nchi, George Saitoti, alisema jeshi litawasaka wafuasi wa kikundi cha waislamu wenye siasa kali, al Shabaab, kokote wa...
-
Maandamano kupinga uroho wa makampuni yamefanywa sehemu mbali mbali za dunia, yakitiwa moyo na maandamano ya wiki mbili sasa yanayofanywa N...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
ALIYEKUWA Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi (DPA) wa Benki Kuu Tanzania (BoT), Amatus Liyumba ambaye anatumikia kifungo cha miaka miwili je...
-
MWANASIASA machachari ambaye pia ni Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samuel Sitta ametangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Mu...
-
Mwanamfalme wa Uingereza Charles na mkewe Camilla, au The Prince of Wales and The Duchess of Cornwall, kama wanavyojulikana rasmi, watafany...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)



0 comments:
Post a Comment