VILIO na simanzi kubwa, jana viligubika katika mazishi ya mtoto mdogo, Teneli Malemi
Mang’ombe (11), aliyeuawa kwa kupigwa risasi na mwenyekiti wa zamani wa CCM Mkoa wa
Mwanza, Clement Mabina.
Mazishi hayo yalifanyika nyumbani kwa marehemu Kitongoji cha Kanyama, Kata ya Kisesa
wilayani Magu mkoani hapa.
Katika ibada ya mazishi hayo iliyoongozwa na Paroko wa Parokia ya Bujora Kisesa, Padri
Fabian Mhoja, akisaidiwa na Katekista wa Parokia hiyo, Faustine Lucas, ilihudhuriwa na
viongozi mbalimbali wa CCM na CHADEMA na serikali wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya
Magu, Jacqueline Liana.
CCM washukuru kutotimuliwa msibani
Akitoa salamu za chama mara baada ya kumalizika maziko ya mtoto huyo aliyekuwa akisoma
darasa la sita Shule ya Msingi Kanyama, Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza, Joyce Masunga
alisema: “Tulishtushwa sana tuliposikia tukio hili. Lakini tunashukuru wazazi, ndugu na jamaa
hamjatufukuza kwenye msiba huu.”
Katibu huyo mbali na kutotoa rambirambi ya fedha, alijivunia chama chake kuandaa chakula
msibani hapo, na yeye kuosha mwili wa marehemu Taneli kwenye chumba cha kuhifadhia
marehemu hospitali ya Bugando.
“Kwa niaba ya chama tawala cha CCM, ninashukuru sana familia ya marehemu maana
hamjatufukuza katika msiba huu. Ingekuwa sehemu nyingine tungeweza kufukuzwa kwa sababu
kiongozi wa CCM amehusika kuua. Ila naomba sana tuweni na upendo, uvumilivu na amani,”
alisema Masunga huku akipiga magoti.
Mkuu wa wilaya hiyo, Jacqueline Liana alisema: “Kila mtu asimamie amani. Tukio kama hili
lisitokee tena katika wilaya yangu hii ya Magu, na ikiwezekana liwe la kwanza na la mwisho
kote nchini. Na Serikali ya Magu inatoa pole ya rambirambi kwa familia ya marehemu ya sh
300,000.”
Taneli aliuawa kwa kupigwa risasi na Mabina kisha nae kuuawa na wananchi papo hapo,
Desemba 15 mwaka huu, katika ugomvi wa mashamba kati yake na wananchi wa Kanyama.
Mazishi ya Mabina yawa gumzo
Wakati huo huo, Mabina ambaye alikuwa diwani wa Kata ya Kisesa wilayani Magu na mjumbe
wa mkutano mkuu wa taifa CCM aliyeuawa na wananchi wenye hasira, anatarajiwa kuzikwa
kesho, ambapo mazishi yake yatagharimu sh milioni 22.
Tetesi zilizopatikana kutoka kwa baadhi ya waombolezaji nyumbani kwa marehemu Mabina,
zinaeleza kwamba, Rais Jakaya Kikwete huenda akaongoza mazishi ya kiongozi huyo.
Baadhi ya wananchi wa Kisesa walionekana kufurahi kuuawa kwa kiongozi huyo, kwa madai
kwamba alikuwa amewasumbua kwa kuwadhulumu mashamba kwa muda mrefu.
MABINA AZIKWA KESHO
Jitokezedirectory
Thursday, December 19, 2013
Popular Posts
-
JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Cha...
-
Rais Dk.Kikwete akisimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wabena katika sherehe za kuzindua mkoa mpya ...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
NEEMA imeendelea kumdondokea mwanamuziki Chaz Baba ambaye baada ya kuhamia Bendi ya Mashujaa Musica na kuvuta mkwanja mrefu, sasa amechag...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Mwanaharakati wa haki za binadamu nchini Kenya Al-Amin Kimathi ni miogoni mwa washukiwa watano wa shambulio la bomu la mjini Kampala wakati...
-
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itafanya kila juhudi kuhakikisha...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo jipya la K...
-
DHANA ya kwamba Tanzania tumekuwa hatufaidi maliasili zetu kama vile utalii, madini , pamoja na mlima Kilimanjaro, na badala yake fursa...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment