MBUNGE wa Ubungo (Chadema), John Mnyika amesema ataongeza nguvu ya wabunge wanaotaka Serikali kuchukua hatua za haraka kuwataja baadhi ya viongozi na wafanyabiashara wanaodaiwa kuficha nje mabilioni ya fedha yanayosadikiwa kupatikana kwa njia isiyo sahihi. Mnyika aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Saranga Mbezi jijini Dar es Salaam, ambapo tayari Mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alishatoa kauli kama hiyo ya kuitaka Serikali kuchukua hatua za haraka kuwataja watu hao kabla ya vikao vya Bunge vya mwezi Aprili. Akizungumza katika mkutano huo, Mnyika alisema Serikali itegemee kupata upinzani mkubwa katika vikao vya Bunge Aprili mwakani kama haita jisafisha kwa kuwataja watu hao na kuwachukulia hatua. “Nia yetu ni kuhakikisha watu wote wanaodaiwa kuwa na akaunti mbalimbali nje ya nchi Serikali inawachukulia hatua pamoja na kuwataja kwa majina ili watanzania waeze kuwafahamu watu wanao wasababisha waishi katika hali ngumu,” alisema Mnyika na kuongeza: “Nijambo la kushangaza kusikia kwamba Serikali ya CCM inasema wapinzani ndiyo tuwataje lakini suala hilo lipo wazi kwani kama itakumbukwa, Septemba 15 mwaka 2010 katika viwanja vya Mwembeyanga tulitaja majina hayo na wengine kwa sasa ndio Viongozi wakubwa ndani ya Bunge.” Mnyika alibainisha kwamba Chadema itaendelea na kasi yake ile ile hadi kuhakikisha viongozi wote wanaodaiwa kuwa na akaunti nje ya nchi wanajulikana wazi ili Watanzania wawafahamu watu wanao tumia kodi zao kwa masilahi yao binafsi. Katika hatua nyingine, Mnyika alisema suala la usafiri katika jiji la Dar es Salaam bado ni tatizo kwani hata kuwapo kwa usafiri wa treni sio suluhisho kutokana na Serikali kupata hasara ya Sh10 milioni kila baada ya siku tano kutokana na undeshaji wa usafiri huo. Alisema kutokana na maandalizi duni Serikali inapata hasara ya Sh10 milioni jambo ambalo ni hatari kwani itafikia hatua usafiri huo wa Treni utasimama. “Ni vyema Serikali ikajipanga vizuri kwani kwa sasa wakazi wengi wa Jiji la Dar es Salaam wanafurahia usafiri wa Treni lakini ipo siku usafiri huo utasimama kutokana na kuendeshwa kwa hasara kubwa,” alisema na kuongeza; “Jambo hilo linatokana na kuwa na miundombinu mibovu na maandalizi duni yaliyofanywa na mawaziri wa uchukuzi waliopita.”
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment