MBUNGE wa Ubungo (Chadema), John Mnyika amesema ataongeza nguvu ya wabunge wanaotaka Serikali kuchukua hatua za haraka kuwataja baadhi ya viongozi na wafanyabiashara wanaodaiwa kuficha nje mabilioni ya fedha yanayosadikiwa kupatikana kwa njia isiyo sahihi. Mnyika aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Saranga Mbezi jijini Dar es Salaam, ambapo tayari Mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alishatoa kauli kama hiyo ya kuitaka Serikali kuchukua hatua za haraka kuwataja watu hao kabla ya vikao vya Bunge vya mwezi Aprili. Akizungumza katika mkutano huo, Mnyika alisema Serikali itegemee kupata upinzani mkubwa katika vikao vya Bunge Aprili mwakani kama haita jisafisha kwa kuwataja watu hao na kuwachukulia hatua. “Nia yetu ni kuhakikisha watu wote wanaodaiwa kuwa na akaunti mbalimbali nje ya nchi Serikali inawachukulia hatua pamoja na kuwataja kwa majina ili watanzania waeze kuwafahamu watu wanao wasababisha waishi katika hali ngumu,” alisema Mnyika na kuongeza: “Nijambo la kushangaza kusikia kwamba Serikali ya CCM inasema wapinzani ndiyo tuwataje lakini suala hilo lipo wazi kwani kama itakumbukwa, Septemba 15 mwaka 2010 katika viwanja vya Mwembeyanga tulitaja majina hayo na wengine kwa sasa ndio Viongozi wakubwa ndani ya Bunge.” Mnyika alibainisha kwamba Chadema itaendelea na kasi yake ile ile hadi kuhakikisha viongozi wote wanaodaiwa kuwa na akaunti nje ya nchi wanajulikana wazi ili Watanzania wawafahamu watu wanao tumia kodi zao kwa masilahi yao binafsi. Katika hatua nyingine, Mnyika alisema suala la usafiri katika jiji la Dar es Salaam bado ni tatizo kwani hata kuwapo kwa usafiri wa treni sio suluhisho kutokana na Serikali kupata hasara ya Sh10 milioni kila baada ya siku tano kutokana na undeshaji wa usafiri huo. Alisema kutokana na maandalizi duni Serikali inapata hasara ya Sh10 milioni jambo ambalo ni hatari kwani itafikia hatua usafiri huo wa Treni utasimama. “Ni vyema Serikali ikajipanga vizuri kwani kwa sasa wakazi wengi wa Jiji la Dar es Salaam wanafurahia usafiri wa Treni lakini ipo siku usafiri huo utasimama kutokana na kuendeshwa kwa hasara kubwa,” alisema na kuongeza; “Jambo hilo linatokana na kuwa na miundombinu mibovu na maandalizi duni yaliyofanywa na mawaziri wa uchukuzi waliopita.”
Popular Posts
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
BAADA ya juzi Jeshi la Polisi kuwahoji na kuwaachulia huru wabunge wa Chadema, jana asubuhi walikamatwa na kutupwa korokoroni hadi kesho ...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasafisha aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi ...
-
UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Maha...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment