Wanasiasa wawili wa Kenya wanaotaraji kugombea uongozi na ambao wameshtakiwa na Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa, ICC, kwa kuchochea fujo baada ya uchaguzi, wametangaza rasmi kuwa wanaungana katika uchaguzi mkuu wa mwaka ujao, Katika mkutano wa hadhara uliofanywa mjini Nakuru makamo wa Waziri Mkuu, Uhuru Kenyatta, alisema atagombea urais na waziri wa zamani, William Ruto, alisema yeye atakuwa mgombea mwenza wa Bwana Kenyatta. Siku ya Ijumaa shirika la Kenya la kutetea haki (the International Centre for Peace and Conflict) lilifikisha kesi mahakama makuu kudai kuwa wanasiasa hao hawafai kushika madaraka. Wanasiasa wengine maarufu wa Kenya piya wameshtakiwa na ICC.
Popular Posts
-
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma ya Bunge ya Hesbu za Mashirika ya Umma, Kabwe Zuberi Zitto, akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma ...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
-
SHOGA AOKOKA NA KUACHANA KABISA NA MASUALA YA USHOGA KUTOKANA NA KAMPENI MAALUM ILIYOENDESHWA NA KANISA LA TANZANIA ASSEMBLIES OF...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment