Dar es Salaam. Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka amesema mwezi ujao wanatarajia kutangaza kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi wa sekta zote.
Akizungumza jana wakati wa mkutano kuhusu sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa Baraza Kuu la Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), alisema kwa muda mrefu kiwango cha kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi wa sekta zote kilikuwa hakijabadilishwa.
“Kwa muda mrefu tulikuwa hatujatangaza kima cha chini cha mshahara, lakini nafurahi kuwajulisha tu kwamba mwezi ujao tutatangaza rasmi,”alisema Kabaka.
Pia alitahadharisha kuhusu utitiri wa vyama katika sehemu moja ya kazi kushauri waajiri wasiruhusu wafanyakazi waanzishe kwa sababu vitakosa nguvu ya kujadiliana na mwajiri katika kufunga mikataba ya hiyari .
Waziri huyo alisema sekta ya hifadhi ya jamii ina idadi ndogo ya wanachama waliojiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii ukilinganisha na idadi ya nguvu kazi iliyopo ambayo ni milioni 22.
Awali Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii, Irene Isaka alisema hadi sasa michango katika mifuko hiyo imefikia Sh 1.4 trilioni na kwamba mafao yanayolipwa yamepanda kutoka Sh500 bilioni hadi kufikia Sh 724 bilioni.
KIMA CHA CHINI CHA MISHAHARA KUTANGANZWA MWEZI UJAO
Jitokezedirectory
Friday, March 29, 2013
Popular Posts
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
RAIS Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo maofisa wakuu kutoka cheo cha Meja Jenerali kuwa Luteni Jenerali kuanzia Novemba 21,mwaka huu. K...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
-
Na Heka Paul na Shakila Galus- MAELEZO- Dar es salaam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuf...
-
MBUNGE wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu Sugu, ameungana na wananchi wanaotaka Katiba Mpya ifute uwepo wa wakuu wa wilaya...
-
Brazil's government has said it will implement 50bn reais ($30bn; £19bn) of spending cuts in order to curb inflation and help prevent t...
-
The rankings of Africa’s top higher education institutions is provided by the 4 International Colleges & Universities (4icu). ...
-
Katika Teknolojia Wiki Hii - Polisi yawasaka watumiaji Blackberry, wadukuzi walenga Blackberry, mashine za kupaa zilizotengenezwa nyumbani ...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment