Mahudhurio ya wajumbe yamkatisha tamaa Dk Slaa
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeeo( Chadema), Dk Willbrod Slaa jana alizungumzia kukatishwa kwake tamaa na mahudhurio ya wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam. Dk Slaa alisema hayo jana wakati wa Mkutano Mkuu wa jimbo hilo baada ya mahudhurio kuwa hafifu. Alisema asilimia 50 ya mahudhurio ya wajumbe katika jimbo hilo ni aibu na yanatia shaka iwapo wana nia ya dhati ya kushika dola mwaka 2015. “Dalili hii inaonyesha kwamba kuna tatizo, hivyo kupitia mkutano huu tutayamaliza na kurudisha ufanisi wa chama” alisema Dk Slaa na kuongeza: “Chadema ni chama ambacho kinajiandaa kushika dola mwaka 2015, endapo hali hii itaendelea ya wajumbe kutafutana kwa njia ya simu itakuwa hatari wakati wa kuunda baraza la mawaziri” alisema na kuongeza: “Haiwezekani Rais akawa anatafuta baraza la mawaziri kwa njia ya simu, kwani bila kujipanga wakati huu itakuwa ngumu huko mbele tunakokwenda,” alisema. Katika mazungumzo yake Dk Slaa alisema, wanakusudia kutoa tamko la nini ifanyike kuhusu mauaji mbalimbali ya wananchi yalifanywa na polisi baada ya Rais Jakaya Kikwete kushindwa kuwachukulia hatua Waziri wa Mambo ya Ndani , Dk Emmanuel Nchimbi, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Saidi Mwema na Kamanda wa Mkoa wa Iringa Michael Kamhanda. “Hatuwezi kutulia huku tukiona vyombo ambavyo vinatakiwa kulinda usalama wa raia ndio vinakuwa vya kwanza kuwaua raia wasiokuwa na hatia huku kiongozi wa nchini (Rais Kikwete) akiwa kimya bila kutoa tamko lolote,” alisema. Katika mkutano huo, wajumbe walitakiwa kufika mapema kwa ajili ya kuanza kwa mkutano saa 4 hadi saa 6 mchana, lakini kutokana na ufinyu wa mahudhurio, mkutano huo ulianza saa 6.47 mchana. Sifa zimwendee Mwenyekiti wa Chama hicho Jimbo la Kinondoni, Deo Mushi ambaye alifanya kazi ya kuwatafuta wajumbe hao kwa njia ya simu ili kutimiza idadi ya asilimia 50. Mratibu wa Mkutano huo, Mkurungenzi wa Sera na Utafiti wa Chama hicho, Chacha Mwita, alisema wajumbe waliokuwa wamefika walikuwa hawana uwezo wa kuruhusu kufanyika kwa mkutano huo. Mwita alisema idadi ambayo inatakiwa ya wajumbe wote ni zaidi ya 120, lakini waliokuwa wamefika walikuwa hawazidi 50.Popular Posts
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
JOSEPH KABILA Ni kijana na anawakilisha mustakabali wa nchi," Ndivyo walivyosema wafuasi wa Joseph Kabila wakati akiwasilisha fomu ...
-
safara wa magari wenye ulinzi na silaha kutoka Libya umevuka mpaka kuingia nchini Niger, ripoti zinasema. Msafara huo unaaminika ni wa w...
-
VYAMA vya CCM na Chadema vipo kwenye maandalizi ya mchakato wa kutafuta muafaka wa mgogoro wa umeya mkoa wa Arusha, baada Msajili wa Vyama ...
-
Mkesha ulofanyika katika uwanja wa Taifa wa mpira katika kuliombea Taifa
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
Company ya Globalwisesoftnet Tanzania, ime sign Contract na Company ya Google pamoja na Microsoft, kwa lengo la kuendeleza na kubuni mbinu ...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
Zaidi ya watu 100 bado hawajulikani walipo, lakini watu 325 walionusurika wameokolewa, kwa mujibu wa waziri wa masuala ya dharura wa Zanz...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment