Mahudhurio ya wajumbe yamkatisha tamaa Dk Slaa
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeeo( Chadema), Dk Willbrod Slaa jana alizungumzia kukatishwa kwake tamaa na mahudhurio ya wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam. Dk Slaa alisema hayo jana wakati wa Mkutano Mkuu wa jimbo hilo baada ya mahudhurio kuwa hafifu. Alisema asilimia 50 ya mahudhurio ya wajumbe katika jimbo hilo ni aibu na yanatia shaka iwapo wana nia ya dhati ya kushika dola mwaka 2015. “Dalili hii inaonyesha kwamba kuna tatizo, hivyo kupitia mkutano huu tutayamaliza na kurudisha ufanisi wa chama” alisema Dk Slaa na kuongeza: “Chadema ni chama ambacho kinajiandaa kushika dola mwaka 2015, endapo hali hii itaendelea ya wajumbe kutafutana kwa njia ya simu itakuwa hatari wakati wa kuunda baraza la mawaziri” alisema na kuongeza: “Haiwezekani Rais akawa anatafuta baraza la mawaziri kwa njia ya simu, kwani bila kujipanga wakati huu itakuwa ngumu huko mbele tunakokwenda,” alisema. Katika mazungumzo yake Dk Slaa alisema, wanakusudia kutoa tamko la nini ifanyike kuhusu mauaji mbalimbali ya wananchi yalifanywa na polisi baada ya Rais Jakaya Kikwete kushindwa kuwachukulia hatua Waziri wa Mambo ya Ndani , Dk Emmanuel Nchimbi, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Saidi Mwema na Kamanda wa Mkoa wa Iringa Michael Kamhanda. “Hatuwezi kutulia huku tukiona vyombo ambavyo vinatakiwa kulinda usalama wa raia ndio vinakuwa vya kwanza kuwaua raia wasiokuwa na hatia huku kiongozi wa nchini (Rais Kikwete) akiwa kimya bila kutoa tamko lolote,” alisema. Katika mkutano huo, wajumbe walitakiwa kufika mapema kwa ajili ya kuanza kwa mkutano saa 4 hadi saa 6 mchana, lakini kutokana na ufinyu wa mahudhurio, mkutano huo ulianza saa 6.47 mchana. Sifa zimwendee Mwenyekiti wa Chama hicho Jimbo la Kinondoni, Deo Mushi ambaye alifanya kazi ya kuwatafuta wajumbe hao kwa njia ya simu ili kutimiza idadi ya asilimia 50. Mratibu wa Mkutano huo, Mkurungenzi wa Sera na Utafiti wa Chama hicho, Chacha Mwita, alisema wajumbe waliokuwa wamefika walikuwa hawana uwezo wa kuruhusu kufanyika kwa mkutano huo. Mwita alisema idadi ambayo inatakiwa ya wajumbe wote ni zaidi ya 120, lakini waliokuwa wamefika walikuwa hawazidi 50.Popular Posts
-
Company ya Globalwisesoftnet Tanzania, ime sign Contract na Company ya Google pamoja na Microsoft, kwa lengo la kuendeleza na kubuni mbinu ...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Arsenal imemsajili winga wa Southampton Alex Oxlade-Chamberlain kwa ada inayoaminika ni paundi milioni 15. Mchezaji huyo mwenye umri wa m...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
Balozi Seif Ai Iddi (kulia) ambaye ni makamu wa pili wa rais wa zanzibar na mbunge wa jimbo la kitope kaskazini unguja akizungumza na spika...
-
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akionyshwa DJ Tasi (kushoto) anavyofanyakazi alipotembelea kituo cha Magic FM akaiwa katika z...
-
Kwa miaka 28 ukuta huo ulitenganisha upande wa mashariki uliokuwa chini ya utawala wa kikoministi na ule uliokuwa sehemu ya Ujerumani Mag...
-
Wazungu wawili raia wa Ujerumani, VEIXLAR MARLM (24), WEIXLER ROLAND (21) wamenusurika kuuawa baada ya kutekwa na watu waliojifanya waendes...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment