KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za nyama ya kuku kutoka nje ya nchi, hasa kutoka Brazil.
Kwa mujibu wa kambi hiyo, uagizaji huo wa kuku ni kinyume cha sheria za nchi na matamko mbalimbali yanayotolewa mara kwa mara bungeni na Serikali.
Suala hilo liliibuliwa bungeni jana na Msemaji wa kambi hiyo, Sylvester Kasulumbai, wakati akiwasilisha maoni ya kambi hiyo kuhusu bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi iliyowasilishwa na waziri wake, Dk David Mathayo David.
Kasulumbai alisema Aprili 5 mwaka huu mkurugenzi huyo alitoa kibali namba 000551 kwa kampuni ya Frostan Ltd ya jijini Dar es Salaam kuagiza tani 27.1 za nyama ya kuku kutoka Brazil.
Alisema Julai 20 mwaka huu, mkurugenzi huyo pia alitoa kibali kingine chenye namba 00000409 kwa Kampuni ya Malik Faraji, kuagiza tani 100 za nyama ya kuku kutoka Zanzibar.
Kwa mujibu wa msemaji huyo, tani hizo 100 za nyama za kuku zilizoagizwa kutoka Zanzibar zilikuwa ni kwa ajili ya migodi ya madini ya Barrick.
“Taarifa zinaonyesha kuwa Tanzania ina kuku takribani milioni 58 wanaofugwa, lakini pamoja na kuku wote hao bado wizara imeendelea kutoa vibali vya kuagiza kuku kutoka Brazil,”alisema.
Kambi hiyo iliitaka Serikali kutoa maelezo kama ni sahihi kuendelea kutoa vibali vya kuagiza kuku kutoka nje ya nchi wakati nchi ina wafugaji
wa kuku.
“Tunataka kujua nyama za kuku kiasi cha tani 100 zilizoagizwa kutoka Zanzibar ni kutoka nchi gani na kama ni kutoka Zanzibar, kwanini wanahitaji kibali kusafirisha nyama kuja bara,”alisema.
Kambi hiyo pia imekilipua kiwanda cha sukari cha Kagera Sugar kwa kutumia ekari 45,000 ilizopewa na Serikali. kulikodisha kwa wafugaji wa Rwanda na Uganda.
Kasulumbai alifafanua kuwa vitalu vya Ranchi ya Kitengule viligawiwa kwa wafugaji wawekezaji wadogo wadogo ambapo kila mmoja alipata kati ya hekta 2,000 na 3,000.
“Lakini cha ajabu kiwanda cha Kagera Sugar kilipewa hekta 45,000 wakati kiwanda hicho hakina mifugo kwa kisingizio tu cha kutaka kulima miwa ndani ya eneo hilo la ufugaji,” alisema.
Kasulumbai alisema kiwanda hicho hivi sasa kinatumia eneo hilo kukodisha wafugaji wa Rwanda na Uganda, ilihali wafugaji wa Tanzania wakikosa eneo la kulishia mifugo yao.
Wapinzani wamlipua Mkurugenzi wa Mifugo
Jitokezedirectory
Friday, August 10, 2012
Popular Posts
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Arsenal imemsajili winga wa Southampton Alex Oxlade-Chamberlain kwa ada inayoaminika ni paundi milioni 15. Mchezaji huyo mwenye umri wa m...
-
ZANZIBAR imo hatarini kukabiliwa na janga kubwa la uharibifu wa mazingira ya bahari iwapo kasi ya uingizaji mifuko ya plastiki itaendelea, ...
-
Tanzania imetangaza kuwa inapiga marufuku biashara ya kukamata na kuwasafirisha wanyamapori kwenda nje ya nchi. Hatua hiyo imetangazwa na...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
Wazalishaji na wasambazaji wa nishati ya gesi kutoka Kisiwa cha Songosongo, SONGAS wameishauri serikali kuwashirikisha wadau wengine ikiwem...
-
Balozi Seif Ai Iddi (kulia) ambaye ni makamu wa pili wa rais wa zanzibar na mbunge wa jimbo la kitope kaskazini unguja akizungumza na spika...
-
MBIO za kuwatafuta vinara watatu wa mastaa wa shindano la Tusker Project Fame, waliowahi kushiriki miaka minne iliyopita zitafikia ukingoni...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)



0 comments:
Post a Comment