MBUNGE wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu Sugu, ameungana na wananchi wanaotaka Katiba Mpya ifute uwepo wa wakuu wa wilaya na mikoa kwa madai kuwa viongozi hao wamewekwa kisiasa zaidi na siyo viongozi wa kiserikali kama inavyodhaniwa hivi sasa. Sugu alitoa mapendekezo hao wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Saza wilayani Chunya mkoani Mbeya kwenye mkutano wa hadhara ambapo alisema kuwa, Katiba ijayo ifute cheo hicho kwani kipo kwa ajili ya kutetea masilahi ya chama tawala na siyo kusimamia rasilimali za Serikali na wananchi wake. Alisema kuwa wakuu wa wilaya na mikoa wangekuwa wapo kama wawakilishi na watendaji wa Serikali kama wanavyodhani walio wengi wasinge kuwa wanashiriki katika shughuli za kisiasa kwani hivi karibuni Chama Cha Mapinduzi(CCM), wakati kikifanya chaguzi za chama hicho viongozi hao pia walikuwa mstari wa mbele katika shughuli za chama hicho. “Ndugu zangu wananchi wa kijiji cha Saza, nasema hivi naungana na wananchi wote waliojitokeza na kutoa maoni yao kwa tume ya kuratibu na kukusanya maoni na kupendekeza kuwa cheo cha mkuu wa mkoa na wilaya kifutwe kwani hawa watu wapo kwa maslahi ya kutetea chama tawala na si vinginevyo,” alisema. Alisema kuwa viongozi hao kwa kuwa hawatambui kazi yao wala nafasi yao ina umuhimu gani kwa wananchi ndiyo maana inafika mahala wanajifanyia mambo watakavyo na kubwa zaidi ni kuendelea kukumbatia shughuli za chama tawala. Mbunge huyo alisema kuwa katika ngazi ya wilaya, shughuli zote zinafanywa na kusimamia na mkurugenzi mtendaji mkuu huku ngazi ya mkoa shughuli zote zinafanywa na kusimamiwa na Katibu tawala wa mkoa hivyo ukiangalia nafasi ya mkuu wa wilaya na mkoa hawana kazi yoyote maalumu.
Popular Posts
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
BAADA ya juzi Jeshi la Polisi kuwahoji na kuwaachulia huru wabunge wa Chadema, jana asubuhi walikamatwa na kutupwa korokoroni hadi kesho ...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasafisha aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi ...
-
UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Maha...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment