MBUNGE wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu Sugu, ameungana na wananchi wanaotaka Katiba Mpya ifute uwepo wa wakuu wa wilaya na mikoa kwa madai kuwa viongozi hao wamewekwa kisiasa zaidi na siyo viongozi wa kiserikali kama inavyodhaniwa hivi sasa. Sugu alitoa mapendekezo hao wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Saza wilayani Chunya mkoani Mbeya kwenye mkutano wa hadhara ambapo alisema kuwa, Katiba ijayo ifute cheo hicho kwani kipo kwa ajili ya kutetea masilahi ya chama tawala na siyo kusimamia rasilimali za Serikali na wananchi wake. Alisema kuwa wakuu wa wilaya na mikoa wangekuwa wapo kama wawakilishi na watendaji wa Serikali kama wanavyodhani walio wengi wasinge kuwa wanashiriki katika shughuli za kisiasa kwani hivi karibuni Chama Cha Mapinduzi(CCM), wakati kikifanya chaguzi za chama hicho viongozi hao pia walikuwa mstari wa mbele katika shughuli za chama hicho. “Ndugu zangu wananchi wa kijiji cha Saza, nasema hivi naungana na wananchi wote waliojitokeza na kutoa maoni yao kwa tume ya kuratibu na kukusanya maoni na kupendekeza kuwa cheo cha mkuu wa mkoa na wilaya kifutwe kwani hawa watu wapo kwa maslahi ya kutetea chama tawala na si vinginevyo,” alisema. Alisema kuwa viongozi hao kwa kuwa hawatambui kazi yao wala nafasi yao ina umuhimu gani kwa wananchi ndiyo maana inafika mahala wanajifanyia mambo watakavyo na kubwa zaidi ni kuendelea kukumbatia shughuli za chama tawala. Mbunge huyo alisema kuwa katika ngazi ya wilaya, shughuli zote zinafanywa na kusimamia na mkurugenzi mtendaji mkuu huku ngazi ya mkoa shughuli zote zinafanywa na kusimamiwa na Katibu tawala wa mkoa hivyo ukiangalia nafasi ya mkuu wa wilaya na mkoa hawana kazi yoyote maalumu.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment