MBUNGE wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu Sugu, ameungana na wananchi wanaotaka Katiba Mpya ifute uwepo wa wakuu wa wilaya na mikoa kwa madai kuwa viongozi hao wamewekwa kisiasa zaidi na siyo viongozi wa kiserikali kama inavyodhaniwa hivi sasa. Sugu alitoa mapendekezo hao wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Saza wilayani Chunya mkoani Mbeya kwenye mkutano wa hadhara ambapo alisema kuwa, Katiba ijayo ifute cheo hicho kwani kipo kwa ajili ya kutetea masilahi ya chama tawala na siyo kusimamia rasilimali za Serikali na wananchi wake. Alisema kuwa wakuu wa wilaya na mikoa wangekuwa wapo kama wawakilishi na watendaji wa Serikali kama wanavyodhani walio wengi wasinge kuwa wanashiriki katika shughuli za kisiasa kwani hivi karibuni Chama Cha Mapinduzi(CCM), wakati kikifanya chaguzi za chama hicho viongozi hao pia walikuwa mstari wa mbele katika shughuli za chama hicho. “Ndugu zangu wananchi wa kijiji cha Saza, nasema hivi naungana na wananchi wote waliojitokeza na kutoa maoni yao kwa tume ya kuratibu na kukusanya maoni na kupendekeza kuwa cheo cha mkuu wa mkoa na wilaya kifutwe kwani hawa watu wapo kwa maslahi ya kutetea chama tawala na si vinginevyo,” alisema. Alisema kuwa viongozi hao kwa kuwa hawatambui kazi yao wala nafasi yao ina umuhimu gani kwa wananchi ndiyo maana inafika mahala wanajifanyia mambo watakavyo na kubwa zaidi ni kuendelea kukumbatia shughuli za chama tawala. Mbunge huyo alisema kuwa katika ngazi ya wilaya, shughuli zote zinafanywa na kusimamia na mkurugenzi mtendaji mkuu huku ngazi ya mkoa shughuli zote zinafanywa na kusimamiwa na Katibu tawala wa mkoa hivyo ukiangalia nafasi ya mkuu wa wilaya na mkoa hawana kazi yoyote maalumu.
Popular Posts
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itafanya kila juhudi kuhakikisha...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
Wazalishaji na wasambazaji wa nishati ya gesi kutoka Kisiwa cha Songosongo, SONGAS wameishauri serikali kuwashirikisha wadau wengine ikiwem...
-
Dar es Salaam. Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka amesema mwezi ujao wanatarajia kutangaza kima cha chini cha mshahara kwa wafany...
-
JAJI MKUU AELEZA SABABU ZA KUJITOA KESI YA LEMA JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji wali...
-
RAIS wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Kikwete, anatarajiwa kuandaa chakula cha hisani Oktoba 18, mwaka huu kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
WAKATI mpango wa mwaka mmoja wa umeme wa dharura ukiwa umemalizika, utekelezaji wake umeshindwa kufikiwa na matokeo yake tatizo la mgaw...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment