Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia ya nchi ya Zanzibar kabla na baada ya Mapinduzi. Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Divisheni ya Makumbusho Zanzibar Khamis Abdallah Ali wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ziara iliyojumuisha wanahabari na maafisa wa Makumbusho Amesema katika kutekeleza agizo la Utalii kwa wote wananchi wanapaswa kushajihishwa kutembelea maeneo ya kihistoria badala ya kuwaachia watalii peke yao kufanya ziara katika maeneo hayo. Amesema ni jambo la kusikitisha kuona wenyeji hawana hamu ya kujua historia ya nchi yao na kuwafanya wageni kujua historia ya Zanzibar kuliko Ameongeza kuwa Idara ya Makumbusho imeweka kiwango kidogo cha Shilingi 1000 ili kumrahisishia mwenyeji pale anapohitaji kwenda kutembelea maeneo ya makumbusho kwa ajili ya kujua historia ya nchi yao
Popular Posts
-
I: UTANGULIZI a) Masuala ya Jumla Mheshimiwa Spika, 1. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi M...
-
Mtaalamu kutoka Finland asaidia mikakati ya tehama
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
JOSEPH KABILA Ni kijana na anawakilisha mustakabali wa nchi," Ndivyo walivyosema wafuasi wa Joseph Kabila wakati akiwasilisha fomu ...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment