Na Heka Paul na Shakila Galus- MAELEZO- Dar es salaam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kufungua Mkutano wa Kimataifa wa wadau wa chanjo duniani (GAVI) utakaonza leo. Mkutano huo unatarajiwa kuwa washiriki 600 kutoka nchi mbalimbali duniani wakiwemo wake wa Marais , Mawaziri wa Afya, fedha na watu mashuhuri kutoka nchi 73. Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana mjini Dar es salaam na Kaimu Katibu Mkuu Regina Kikuli inasema kuwa lengo la mkutano huo ni pamoja na kujadili mafanikio na changamoto zinakabili huduma ya utoaji wa chanjo duniani. Taarifa hiyo inaongeza kuwa hii ni mara ya kwanza mkutano wa aina hiyo kufanyika Afrika mashariki na kuongeza kuwa sababu zilizopelekea mkutano kufanyika Tanzania ni pamoja na mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma za chanjo za watoto na mama wajawazito. Hivyo basi washiriki watapata fursa ya kutembelea vituo vinavyotoa huduma za chanjo nchini ili kujionea mafanikio na changamoto zilizopo pamoja na kujifunza. Vilevile washiriki watapata fursa ya kujadili masuala ya chanjo ikiwemo uingizwaji wa chanjo mpya na masuala ya afya ya mama na mtoto. Pia kutakuwepo na uzinduzi wa chanjo mbili mpya za magonjwa ya kuhara, homa ya uti wa mgongo kwa watoto chini ya mwaka mmoja ambazo zinatolewa nchini kwa hisani GAVI.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment