Na Heka Paul na Shakila Galus- MAELEZO- Dar es salaam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kufungua Mkutano wa Kimataifa wa wadau wa chanjo duniani (GAVI) utakaonza leo. Mkutano huo unatarajiwa kuwa washiriki 600 kutoka nchi mbalimbali duniani wakiwemo wake wa Marais , Mawaziri wa Afya, fedha na watu mashuhuri kutoka nchi 73. Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana mjini Dar es salaam na Kaimu Katibu Mkuu Regina Kikuli inasema kuwa lengo la mkutano huo ni pamoja na kujadili mafanikio na changamoto zinakabili huduma ya utoaji wa chanjo duniani. Taarifa hiyo inaongeza kuwa hii ni mara ya kwanza mkutano wa aina hiyo kufanyika Afrika mashariki na kuongeza kuwa sababu zilizopelekea mkutano kufanyika Tanzania ni pamoja na mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma za chanjo za watoto na mama wajawazito. Hivyo basi washiriki watapata fursa ya kutembelea vituo vinavyotoa huduma za chanjo nchini ili kujionea mafanikio na changamoto zilizopo pamoja na kujifunza. Vilevile washiriki watapata fursa ya kujadili masuala ya chanjo ikiwemo uingizwaji wa chanjo mpya na masuala ya afya ya mama na mtoto. Pia kutakuwepo na uzinduzi wa chanjo mbili mpya za magonjwa ya kuhara, homa ya uti wa mgongo kwa watoto chini ya mwaka mmoja ambazo zinatolewa nchini kwa hisani GAVI.
Popular Posts
-
JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Cha...
-
Rais Dk.Kikwete akisimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wabena katika sherehe za kuzindua mkoa mpya ...
-
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya waombolezaji baada a kuwasili nyumbani kwa aliyekuwa Wazri wa Fedha, Dr. ...
-
MFUMUKO wa bei unaweza kuwakimbiza wawekezaji wanaotaka kuja nchini kuwekeza rasilimali zao kama utaendelea kukua kama ilivyo sasa.Kwa s...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), imezikutanisha kampuni za mafuta hapa nchini kwa lengo kuunda Bodi ya Wakurugenzi ya Kampu...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo jipya la K...
-
DHANA ya kwamba Tanzania tumekuwa hatufaidi maliasili zetu kama vile utalii, madini , pamoja na mlima Kilimanjaro, na badala yake fursa...
-
Ujerumani imerejesha mafuvu ya Wanambia ishirini waliofariki dunia baada ya fujo dhidi ya utawala wa ukoloni wa Kijerumani zaidi ya miaka 1...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment