Na Heka Paul na Shakila Galus- MAELEZO- Dar es salaam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kufungua Mkutano wa Kimataifa wa wadau wa chanjo duniani (GAVI) utakaonza leo. Mkutano huo unatarajiwa kuwa washiriki 600 kutoka nchi mbalimbali duniani wakiwemo wake wa Marais , Mawaziri wa Afya, fedha na watu mashuhuri kutoka nchi 73. Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana mjini Dar es salaam na Kaimu Katibu Mkuu Regina Kikuli inasema kuwa lengo la mkutano huo ni pamoja na kujadili mafanikio na changamoto zinakabili huduma ya utoaji wa chanjo duniani. Taarifa hiyo inaongeza kuwa hii ni mara ya kwanza mkutano wa aina hiyo kufanyika Afrika mashariki na kuongeza kuwa sababu zilizopelekea mkutano kufanyika Tanzania ni pamoja na mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma za chanjo za watoto na mama wajawazito. Hivyo basi washiriki watapata fursa ya kutembelea vituo vinavyotoa huduma za chanjo nchini ili kujionea mafanikio na changamoto zilizopo pamoja na kujifunza. Vilevile washiriki watapata fursa ya kujadili masuala ya chanjo ikiwemo uingizwaji wa chanjo mpya na masuala ya afya ya mama na mtoto. Pia kutakuwepo na uzinduzi wa chanjo mbili mpya za magonjwa ya kuhara, homa ya uti wa mgongo kwa watoto chini ya mwaka mmoja ambazo zinatolewa nchini kwa hisani GAVI.
Popular Posts
-
NEW YORK, Marekani VIDEO iliyoonyweshwa mwishoni mwa wiki katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ambayo ilielezea madhara ya taratibu ana...
-
RAIS Jakaya Kikwete ameeleza mikakati ya Serikali yake kuwa ni kuhakikisha inamaliza kabisa maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi ifikapo...
-
Uingereza imesitisha kwa muda msaada iliyokuwa iipe Rwanda kwa sababu ya wasiwasi kuhusu kuhusika kwa nchi hiyo katika mzozo uliopo Jam...
-
BAADA ya juzi Jeshi la Polisi kuwahoji na kuwaachulia huru wabunge wa Chadema, jana asubuhi walikamatwa na kutupwa korokoroni hadi kesho ...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
HERIETH MAKWETTA MSANII wa muziki wa kizazi kipya kutoka Tanzania, Rehema Chalamila maarufu kama Ray C, yupo katika kituo maalumu cha msa...
-
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imewasafisha aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Ofisa Utawala wa ubalozi ...
-
UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Maha...
-
Wananchi wameshauriwa kutekeleza agizo la Utalii kwa wote kwa kuyatembelea maeneo mbali mbali ya utalii Zanzibar ili kufahamu historia y...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment