MKAZI wa Kijiji cha Kilombero, mkoani Geita, Mahangaiko Buruhe (52) amefariki dunia baada ya kusombwa na upepo mkali ulioambatana na mvua wakati akijaribu kuzuia nyumba yake isianguke. Tukio hilo lilitokea juzi saa 10;00 jioni ambapo marehemu alikuwa akizuia nyumba yake isisombwe na upepo baada ya kushuhudia paa la nyumba likiezuliwa na upepo. Marehemu aliamua kurukia kenchi ili kuzua nyumba isianguke kwa kutumia nguvu zake na kwamba upepo ulimzidi nguvu, paa likaezuliwa na marehemu kurushwa nje na kuangukia nyumba ya pili alikopoteza maisha. Mashuhuda wa tukio hilo Makwiwa Bihalale (mke wa marehemu) na Chausiku Malole walisema marehemu alikuwa akifanya juhudi za kuokoa nyumba isianguke na upepo ndipo mauti yakamkuta hali ambayo imewashtua. Akizungumza mbele ya viongozi waliotembelea hapo kuona tukio hilo, Kaimu Ofisa Tarafa ya Busanda, Joseph Kaparatus alisema tukio hilo lilitokana na ujenzi mbovu wa nyumba hiyo na kwamba iliezekwa bila kuzingatia utaalamu na haina kenchi zaidi ya mbao ambazo zimegongelewa bati. “Nyumba hii ilikuwa na uhalali wa kuanguka mkuu, angalia haijajengwa kwa kuzingatia utaalamu wa ujenzi wa nyumba,” alisema Kaparatus. Awali akizungumza na wakazi wa eneo hilo nyumbani kwa marehemu Mkuu wa Wilaya ya Geita, Said Mangochie aliwataka wanachi hao kujenga nyumba bora zinazozingatia utaalamu ili kuepusha majanga wakati wa mvua. Mwenyekiti wa kijiji hicho Haruna Shabani alisema marehemu aliwahi kuwa mtendaji wa kijiji, na kiongozi wa CCM Kata ya Busanda, ameacha wajane wawili na watoto 18.
Popular Posts
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Arsenal imemsajili winga wa Southampton Alex Oxlade-Chamberlain kwa ada inayoaminika ni paundi milioni 15. Mchezaji huyo mwenye umri wa m...
-
ZANZIBAR imo hatarini kukabiliwa na janga kubwa la uharibifu wa mazingira ya bahari iwapo kasi ya uingizaji mifuko ya plastiki itaendelea, ...
-
Tanzania imetangaza kuwa inapiga marufuku biashara ya kukamata na kuwasafirisha wanyamapori kwenda nje ya nchi. Hatua hiyo imetangazwa na...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
Wazalishaji na wasambazaji wa nishati ya gesi kutoka Kisiwa cha Songosongo, SONGAS wameishauri serikali kuwashirikisha wadau wengine ikiwem...
-
Balozi Seif Ai Iddi (kulia) ambaye ni makamu wa pili wa rais wa zanzibar na mbunge wa jimbo la kitope kaskazini unguja akizungumza na spika...
-
MBIO za kuwatafuta vinara watatu wa mastaa wa shindano la Tusker Project Fame, waliowahi kushiriki miaka minne iliyopita zitafikia ukingoni...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment