MKAZI wa Kijiji cha Kilombero, mkoani Geita, Mahangaiko Buruhe (52) amefariki dunia baada ya kusombwa na upepo mkali ulioambatana na mvua wakati akijaribu kuzuia nyumba yake isianguke. Tukio hilo lilitokea juzi saa 10;00 jioni ambapo marehemu alikuwa akizuia nyumba yake isisombwe na upepo baada ya kushuhudia paa la nyumba likiezuliwa na upepo. Marehemu aliamua kurukia kenchi ili kuzua nyumba isianguke kwa kutumia nguvu zake na kwamba upepo ulimzidi nguvu, paa likaezuliwa na marehemu kurushwa nje na kuangukia nyumba ya pili alikopoteza maisha. Mashuhuda wa tukio hilo Makwiwa Bihalale (mke wa marehemu) na Chausiku Malole walisema marehemu alikuwa akifanya juhudi za kuokoa nyumba isianguke na upepo ndipo mauti yakamkuta hali ambayo imewashtua. Akizungumza mbele ya viongozi waliotembelea hapo kuona tukio hilo, Kaimu Ofisa Tarafa ya Busanda, Joseph Kaparatus alisema tukio hilo lilitokana na ujenzi mbovu wa nyumba hiyo na kwamba iliezekwa bila kuzingatia utaalamu na haina kenchi zaidi ya mbao ambazo zimegongelewa bati. “Nyumba hii ilikuwa na uhalali wa kuanguka mkuu, angalia haijajengwa kwa kuzingatia utaalamu wa ujenzi wa nyumba,” alisema Kaparatus. Awali akizungumza na wakazi wa eneo hilo nyumbani kwa marehemu Mkuu wa Wilaya ya Geita, Said Mangochie aliwataka wanachi hao kujenga nyumba bora zinazozingatia utaalamu ili kuepusha majanga wakati wa mvua. Mwenyekiti wa kijiji hicho Haruna Shabani alisema marehemu aliwahi kuwa mtendaji wa kijiji, na kiongozi wa CCM Kata ya Busanda, ameacha wajane wawili na watoto 18.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment