UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, bado haujakamilika. Hayo yalielezwa jana na Wakili wa Serikali, Keneth Sekwao wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa na kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika au la. Sekwao alidai mahakamani hapo kuwa, upelelezi haujakamilika na kuomba ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa. Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Mmbando aliiahirisha kesi hiyo hadi Desemba 17, mwaka huu. Lulu anatuhumiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba. Anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 7, 2012 nyumbani kwa marehemu, Sinza Dar es Salaam. Hata hivyo, umri wake ulizua mvutano mkali baina ya upande wa mashtaka katika kesi hiyo na jopo la mawakili wanaomtetea, mvutano ambao ulianzia Mahakama ya Kisutu na kuendelea hadi Mahakama ya Rufani, huku kesi ya msingi ikiwa haijaanza kusikilizwa. Juni 11, mwaka huu Mahakama Kuu ilikubali kufanya uchunguzi wa umri halali wa mshtakiwa, kufuatia maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na jopo la mawakili wanaomtetea Lulu. Upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda, akisaidiana na Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro waliwasilisha maombi Mahakama ya Rufani wakiomba ifanye marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu, kama ulikuwa sahihi. Jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani lililoongozwa na January Msoffe, Jaji Bernard Luanda na Edward Rutakangwa, lilizima mvutano na likaamuru kuendelea kwa kesi ya msingi. Katika uamuzi uliosomwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Zahra Maruma, jopo hilo kwanza lilisema maombi ya marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu, yaliyowasilishwa na Jamhuri yalikuwa batili.
Popular Posts
-
JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji waliopangwa kusikiliza kesi ya aliyekuwa mbunge wa Cha...
-
Rais Dk.Kikwete akisimikwa rasmi kuwa chifu wa kabila la wabena katika sherehe za kuzindua mkoa mpya ...
-
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya waombolezaji baada a kuwasili nyumbani kwa aliyekuwa Wazri wa Fedha, Dr. ...
-
MFUMUKO wa bei unaweza kuwakimbiza wawekezaji wanaotaka kuja nchini kuwekeza rasilimali zao kama utaendelea kukua kama ilivyo sasa.Kwa s...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), imezikutanisha kampuni za mafuta hapa nchini kwa lengo kuunda Bodi ya Wakurugenzi ya Kampu...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifungua pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo jipya la K...
-
DHANA ya kwamba Tanzania tumekuwa hatufaidi maliasili zetu kama vile utalii, madini , pamoja na mlima Kilimanjaro, na badala yake fursa...
-
Ujerumani imerejesha mafuvu ya Wanambia ishirini waliofariki dunia baada ya fujo dhidi ya utawala wa ukoloni wa Kijerumani zaidi ya miaka 1...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment