UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, bado haujakamilika. Hayo yalielezwa jana na Wakili wa Serikali, Keneth Sekwao wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa na kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika au la. Sekwao alidai mahakamani hapo kuwa, upelelezi haujakamilika na kuomba ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa. Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Mmbando aliiahirisha kesi hiyo hadi Desemba 17, mwaka huu. Lulu anatuhumiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba. Anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 7, 2012 nyumbani kwa marehemu, Sinza Dar es Salaam. Hata hivyo, umri wake ulizua mvutano mkali baina ya upande wa mashtaka katika kesi hiyo na jopo la mawakili wanaomtetea, mvutano ambao ulianzia Mahakama ya Kisutu na kuendelea hadi Mahakama ya Rufani, huku kesi ya msingi ikiwa haijaanza kusikilizwa. Juni 11, mwaka huu Mahakama Kuu ilikubali kufanya uchunguzi wa umri halali wa mshtakiwa, kufuatia maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na jopo la mawakili wanaomtetea Lulu. Upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda, akisaidiana na Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro waliwasilisha maombi Mahakama ya Rufani wakiomba ifanye marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu, kama ulikuwa sahihi. Jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani lililoongozwa na January Msoffe, Jaji Bernard Luanda na Edward Rutakangwa, lilizima mvutano na likaamuru kuendelea kwa kesi ya msingi. Katika uamuzi uliosomwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Zahra Maruma, jopo hilo kwanza lilisema maombi ya marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu, yaliyowasilishwa na Jamhuri yalikuwa batili.
Popular Posts
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
SERIKALI itatoa leseni kwa wafanyabiashara wa hapa nchini, ili kuwawezesha kuagiza tani 120,000 za sukari kutoka nje ya nchi na sukari hiyo...
-
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itafanya kila juhudi kuhakikisha...
-
Huduma ya Maji na Nishati (EWURA), Mhandisi Godwin Samwel, akizungumza na wanahabari jana jijini, Dar es Salaam kuhusu kupanda kwa bei za m...
-
Wazalishaji na wasambazaji wa nishati ya gesi kutoka Kisiwa cha Songosongo, SONGAS wameishauri serikali kuwashirikisha wadau wengine ikiwem...
-
Dar es Salaam. Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka amesema mwezi ujao wanatarajia kutangaza kima cha chini cha mshahara kwa wafany...
-
JAJI MKUU AELEZA SABABU ZA KUJITOA KESI YA LEMA JAJI Mkuu, Mohamed Chande Othman ameeleza sababu za kutokuwa kwenye jopo la majaji wali...
-
RAIS wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Kikwete, anatarajiwa kuandaa chakula cha hisani Oktoba 18, mwaka huu kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa...
-
Mchungaji Lutumba na mkewe wasimikwa kuwa Maaskofu Na Salesi Malula Hayawi hayawi sasa yamekua ndivyo ilivyokuwa siku ya jumap...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment