UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, bado haujakamilika. Hayo yalielezwa jana na Wakili wa Serikali, Keneth Sekwao wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa na kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika au la. Sekwao alidai mahakamani hapo kuwa, upelelezi haujakamilika na kuomba ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa. Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Mmbando aliiahirisha kesi hiyo hadi Desemba 17, mwaka huu. Lulu anatuhumiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba. Anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 7, 2012 nyumbani kwa marehemu, Sinza Dar es Salaam. Hata hivyo, umri wake ulizua mvutano mkali baina ya upande wa mashtaka katika kesi hiyo na jopo la mawakili wanaomtetea, mvutano ambao ulianzia Mahakama ya Kisutu na kuendelea hadi Mahakama ya Rufani, huku kesi ya msingi ikiwa haijaanza kusikilizwa. Juni 11, mwaka huu Mahakama Kuu ilikubali kufanya uchunguzi wa umri halali wa mshtakiwa, kufuatia maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na jopo la mawakili wanaomtetea Lulu. Upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda, akisaidiana na Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro waliwasilisha maombi Mahakama ya Rufani wakiomba ifanye marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu, kama ulikuwa sahihi. Jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani lililoongozwa na January Msoffe, Jaji Bernard Luanda na Edward Rutakangwa, lilizima mvutano na likaamuru kuendelea kwa kesi ya msingi. Katika uamuzi uliosomwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Zahra Maruma, jopo hilo kwanza lilisema maombi ya marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu, yaliyowasilishwa na Jamhuri yalikuwa batili.
Popular Posts
-
What to do in Zanzibar when you’re a tourist? I had booked myself a 4-day trip to the island, and, taking the advice of friends and a quic...
-
RAIS Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo maofisa wakuu kutoka cheo cha Meja Jenerali kuwa Luteni Jenerali kuanzia Novemba 21,mwaka huu. K...
-
KUTOKANA na kile kichoonekana ni kutaka kukabiliana na uhaba wa sukari na kupanda kwa bei yake, Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatarajia kukuta...
-
Na Heka Paul na Shakila Galus- MAELEZO- Dar es salaam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuf...
-
MBUNGE wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu Sugu, ameungana na wananchi wanaotaka Katiba Mpya ifute uwepo wa wakuu wa wilaya...
-
Brazil's government has said it will implement 50bn reais ($30bn; £19bn) of spending cuts in order to curb inflation and help prevent t...
-
The rankings of Africa’s top higher education institutions is provided by the 4 International Colleges & Universities (4icu). ...
-
Katika Teknolojia Wiki Hii - Polisi yawasaka watumiaji Blackberry, wadukuzi walenga Blackberry, mashine za kupaa zilizotengenezwa nyumbani ...
-
WAMILIKI wa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans jana walitoka mahakamani kwa furaha baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutupilia mba...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)
0 comments:
Post a Comment