UPELELEZI wa kesi inayomkabili Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, anayekabiliwa na kesi ya mauaji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, bado haujakamilika. Hayo yalielezwa jana na Wakili wa Serikali, Keneth Sekwao wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa na kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika au la. Sekwao alidai mahakamani hapo kuwa, upelelezi haujakamilika na kuomba ipangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa. Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Mmbando aliiahirisha kesi hiyo hadi Desemba 17, mwaka huu. Lulu anatuhumiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba. Anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 7, 2012 nyumbani kwa marehemu, Sinza Dar es Salaam. Hata hivyo, umri wake ulizua mvutano mkali baina ya upande wa mashtaka katika kesi hiyo na jopo la mawakili wanaomtetea, mvutano ambao ulianzia Mahakama ya Kisutu na kuendelea hadi Mahakama ya Rufani, huku kesi ya msingi ikiwa haijaanza kusikilizwa. Juni 11, mwaka huu Mahakama Kuu ilikubali kufanya uchunguzi wa umri halali wa mshtakiwa, kufuatia maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na jopo la mawakili wanaomtetea Lulu. Upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Elizabeth Kaganda, akisaidiana na Wakili wa Serikali, Shadrack Kimaro waliwasilisha maombi Mahakama ya Rufani wakiomba ifanye marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu, kama ulikuwa sahihi. Jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufani lililoongozwa na January Msoffe, Jaji Bernard Luanda na Edward Rutakangwa, lilizima mvutano na likaamuru kuendelea kwa kesi ya msingi. Katika uamuzi uliosomwa na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Zahra Maruma, jopo hilo kwanza lilisema maombi ya marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu, yaliyowasilishwa na Jamhuri yalikuwa batili.
Popular Posts
-
Nchi kubwa na yenye rasilimali nyingi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imekuwa katika kile kinachotajwa kuwa vita vya Dunia vya Afri...
-
Rap icon Tupac Shakur covers the latest issue of XXL in a profile that celebrates the rapper, who passed away 15 years ago. In the latest...
-
Global wise softnet company is Just providing web hosting for $ 100 per year, contact for your web hosting/ Email; globalwisesoftnet@gma...
-
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amekanusha vikali madai kwamba alishinda uchaguzi wa nchi hiyo kupitia wizi wa kura...
-
WIZARA ya Nishati na Madini, imesema tatizo la umeme nchini linatokana na kuchoka kwa miundombinu na hivyo kuzidiwa nguvu. Kauli hiyo ...
-
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema moja ya mambo yaliyohojiwa na wananchi wengi katika mchaka...
-
US Vice-President Joe Biden has told his Chinese counterpart Xi Jinping that global economic stability rests on the US and China finding co...
-
Katika kuitikia kaulimbiu ya kilimo kwanza Kampuni ya Utalii ya Cordial Tours Yenye makao makuu yake Jijini Dar es salaam imeamua kuunga Mk...
-
President Robert Mugabe scoffed Saturday at calls for him to retire, saying he will remain in power until his Zanu PF party wins elections...
-
KAMBI ya Upinzani Bungeni, jana ilimlipua Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Mifugo, Dk E. J. Sekidio kwa kutoa vibali vya kuagiza tani 127 za ny...
Habari Leo Tanzania, Media, (East Africa)




0 comments:
Post a Comment